0
Baadhi ya matukio katika picha wakati wa kuhitimisha mafunzo ya walimu wanaojiandaa kufanikisha mafunzo ya Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa mtaala ulioboreshwa kwa nchi nzima kwa wanafunzi wa darasa la tatu na nne. 




PHOTO: Naibu waziri wa Elimu na Ufundi Injinia Stella Manyanya akiweka saini kwenye kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika chuo cha Ualimu Bustani Kondoa.

PHOTO: Naibu waziri Injinia Stella Manyanya (katikati) akiwa na viongozi wa mkoa wa Dodoma, mkuu wa wilaya ya Kondoa Kijazi (wa pili kushoto), viongozi wa mafunzo, Mkuu wa chuo cha Bustani wakielekea Ukumbuni kuhitimisha mafunzo ya Awali kwa walimu.


PHOTO: Wahitimu wapatao 444 ambao walihitimu mafunzo ya Kusoma, Kuandika na Kuhesabu pamoja na Kuchopeka wakiwa makini kufuatilia kile kinachoendelea wakati wa kuhitimisha mafunzo hayo.

PHOTO: Dr. Siston Masanja, ambaye ni Mtendaji mkuu wa ADEM akitoa taarifa fupi ya mafunzo tangu yalipoanza na kuhitimishwa kwake ambapo jumla ya washiriki 444 walihitimu mafunzo, kulia kwake ni mkuu wa chuo wa Bustani.

PHOTO: Sehemu ya sherehe yoyote ni nyimbo na furaha, (Kwaya) Walimu wakiimba wimbo wa kushukuru kupata mafunzo na kuonyesha hamasa kwenda kuyatumia kwa walengwa ambao ni wanafunzi wa darasa la 3 na 4.

PHOTO: Baadhi ya walimu wakipiga makofi mara kutokana na wimbo ulioimbwana kwaya ya walimu katika sherehe hiyo. 

PHOTO: Kaimu Mkurugenzi mkuu, Taasisi ya Elimu Tanzania Dr. Elia Kibga akitoa ufafanuzi kuhusu umuhimu wa mafunzo hayo huku akigusia kuhusu ubora wa mafunzo hayo kwa mwanafunzi atakayemaliza awe mwanafunzi bora na si bora mwanafunzi.


PHOTO: Baadhi ya walimu wakifuatilia hotuba kutoka kwa kaimu mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Elimu nchini Elia Kibga (pichani juu)

PHOTO: Mratibu wa Mafunzo kituo cha kutolea Mafunzo cha Bustani Kondoa Luca Mzelela akiongea wakati wa kumkaribisha Naibu waziri kufunga mafunzo hayo, kushoto kwake ni Naibu waziri Stella Manyanya na Mkuu wa wilaya ya Kondoa Kijazi.

PHOTO:  Naibu Waziri wa Elimu Injinia Stella Manyanya akisisitiza kuhusu mafunzo hayo ambayo ni nadra kutokea kwa walimu kutokana na ufinyu wa Bajeti, wakati wa kuhitimisha mafunzo ya awali kwa walimu wa shule za msingi nchini katika kituo cha Bustani Kondoa, kulia kwake ni Mkuu wa wilaya ya Kondoa -Kijazi.

PHOTO: Wawezeshaji wanaotoa mafunzo ya KKK na Uchopekaji wakimsikiliza Naibu waziri Injinia Manyanya wakati akihitimisha mafunzo hayo ya awamu ya kwanza.


PHOTO: Naibu waziri Stella Manyanya (kulia) akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu wa mafunzo Nurdin Ibrahim ikiwa ni kumbumbuku ya kuhitimu.

PHOTO: Naibu waziri Stella Manyanya (kulia) akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Zauda Hussein cheti cha kuhitimu mafunzo.

PHOTO: Picha ya pamoja kwa mgeni rasmi akiwa na viongozi wa ADEM na watoa mafunzo mara maada ya kuhitimishwa kwa mafunzo ya awamu ya kwanza yaliyofsnyika mkoani Dodoma katika wilaya ya Kondoa kwenye chuo cha Ualimu Bustani.

  

Picha: TODAYS PRODUCTION


Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top