![]() |
PHOTO: Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amosi Makalla akiongea
wakati wa uzindizu wa kampeni ya wananchi kutoa maoni.
|
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Amos Makalla amezindua zoezi la wananchi kutoa maoni juu ya migogoro ya Aridhi na mipaka ya vijiji 34 pamoja na hifadhi ya Ruaha ambapo katika uzinduzi huo alifanya mikutano kadhaa katika vijiji kadhaa kikiwepo kijiji cha Igava kata ya Igava wilaya ya Mbalali mkoani Mbeya.
Katika uzinduzi
huo ametambulisha timu mbili za wataalam watakaopita katika vijiji hivyo 34
kupokea maoni ya wananchi ikiwa ni baada
ya wananchi kulalamika kuwa mwaka 2008 wakati serikali inatangaza mipaka
wananchi hao hawakushirikishwa, ambapo kupitia mkutano huo mkuu huyo wa mkoa
amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi pale ambapo kamati hiyo itakuwa inapita
katika vijiji vyao.
Baada ya wananchi kutoa maoni baraza la madiwani,
kamati ya ushauri ya wilaya watatoa maoni na baadaye kamati ya ushauri mkoa na
hatimaye kuwasilishwa kwa muheshimiwa Rais kwa ajili ya maamuzi.
RC Makala amewaonya wale watakaohujumu zoezi hilo
muhimu kwani lengo la zoezi hilo ni kuondoa mgogoro na hifadhi lakini utasaidia
kuboresha ekolojia ya hifadhi ya Ruaha.
Wakati huo huo Mkuu wa
mkoa wa Mbeya Amos Makala amewaomba waviongozi wa dini na Kimila kusaidia
kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwa ajili vya uraia pia kuwaepusha na Imani potofu,
ambapo amewaomba viongozi hao kuhamasisha wananchi kujiandikisha kwa ajili ya
vitambulisho vya Uraia huku akiwataka viongozi kuwa macho na watu wasiokuwa
Raia kuweza kuandikishwa kutokana na Mkoa huo kuwa mpakani hali inayoweza kutoa
fulsa wasio raia kujiandikisha.
![]() |
PHOTO: Mkuu
wa mkoa wa Mbeya Amosi Makalla mwenye suti na tai nyekundu akiwa na baadhi ya
viongozi mbalimbali mkoani Mbeya.
|


Post a Comment