0
Uongozi wa mkoa wa Mara umeshauliwa kuangalia umuhimu wa kuweka mpango shirikishi wa muda mrefu utakaoweza kusaidia watoto walio nje ya mfumo wa shule ndani ya mkoa huo ili waweze kupata elimu stahiki.


PHOTO PROFILE: Graca Machel.




MUSOMA.
Ushuri huo umetolewa na Graca Machel aliyewahi kuwa mke wa Rais wa msumbiji hayati Samora Machel pia baadaye alikuwa mke wa aliyepata kuwa Rais wa Afrika kusini Nelson Mandera, ambapo aliwasili mkoani humo machi 13 kwa ziara ya siku tatu mkoani Mara kuangalia maendeleo ya mradi wa kusaidia watoto walio nje ya mfumo wa Elimu, unaotekelezwa na taasisi yake.

Mama Machel alitoa ushauli huo wakati wa mkutani maalum na wadau ambapo katika mkutano uliotumika kutoa matokeo ya utafiti wa watoto ambao wapo nje ya mfumo wa shule. Pia utafiti huo umebaini watoto wapatao 11,666 wenye umri kati ya miaka 7 hadi 17 wapo nje ya mfumo wa shule chini ya mradi wa miaka miwili ambao unatekelezwa na taasisi ya Graca Machel Trust kwa ushirikiano na Mara Alliance na Serikali ya mkoa kwa Mara.


PHOTO: Mama Graca Machel (wa pili kushoto) akiongoza na Askofu Michael Msongazila wa jimbo la musoma na Mwenyekiti wa Alliance.

“Tunahitaji mpango wa miaka mitano au kumi na tano ili kuondoa ili tatizo na huu ni mwanzo wa safari kuondoa tatizo la watoto ambao wako nje ya mfumo wa shule” alisema Mama Graca Machel.

Pia utafiti huo umeonyeshwa katika halmashauli tano za wilaya za Tarime, Bunda Musoma na Butiama, kupitia wilaya Bunda umeonyesha inaongoza kuwa na watoto wengi walio nje ya shule kwa asilimia 33, Tarime (31), Butiama (26) na M usoma (10). Mkuu wa kitengo cha utafiti na machapisho ya utafiti wa masuala ya uchumi na Jamii (ESRF) ambao wamefanya utafiti huo Dkt Fortunata Makene alisema, utafiti huo umefanyika nyumba kwa nyumba.

Dr. Makene alisema ni muhimu kuwepo na mpango wa kukabiliana na tatizo la ndoa za utotoni katika mkoa wa Mara.

Kwa upande wake mdau wa elimu mkoani Mara, Askofu wa kanisa katoliki jimbo la Musoma Michael Msonganzila alisema kuwa , ni habari njema kuona GMT , Mara Alliance na Serikali wameungana kusaidia watoto ambao wako nje ya mfumo wa elimu ya shule chini ya mpango wa Memkwa.

Akizungumza katika hafla hiyo kaimu mkuu wa mkoa wa Mara , Dr Vicent Naano alimhakikishia mama Graca kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kuhakikisha kuwa tatizo la watoto walio nje ya mfumo wa shule linabaki kuwa historia na kufanya mradi huo kuwa wa mafanikio makubwa.





Chanzo: Habari Leo.

Post a Comment

 
Top