0
PROFILE PHOTO: Rais John Pombe Magufuri.
Mmoja wa wahasisi wa Uhuru na aliyewahi kuwa mmoja wa watendaji wakuu katika serikali ya Tanganyika Sir George Kahama amefariki dunia Jumapili iliyopita akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akitibiwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyothibitishwa na ofisa uhusiano wa hosptali hiyo.

Rais John Magufuli alituma salamu kwa wafiwa pamoja na rambirambi zake kwa familia akisema taifa limempoteza mmoja wa watu muhimu na aliyetoa mchango mkubwa katika kupigania uhuru, maendeleo na ustawi wa jamii ya watanzania. Pia Dkt Magufuli amewapa pole wanachama wote wa CCM, wabunge, ndugu, na marafiki pamoja na wote walioguswa na msiba huo.

Dkt Magufuli amesema, "Sir George alikuwa kiongozi mzalendo,shupavu na mwanasiasa mahiri, aliyewapenda watanzania lakini pia alijitoa kushirikiana na viongozi wenzake akiwemo Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius Nyerere pia alipigania uhuru, kujenga misingi ya taifa likiwemo Azimio la Arusha ikiwemo kujenga misingi ya uchumi wa ujamaa na kujetegemea, kwa hakika hatutamsahau"

Post a Comment

 
Top