0
DAR ES SALAAM.
Kabla ya uzinduzi na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara za mwingiliano na kupishana (frying over/Interchange) kwenye eneo la Ubungo muda mfupi uliopita Rais Magufuri aliwaelezea watanzania yaliyofikiwa ndani ya kipindi chake cha uongozi aliopo ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu waliokuwa wanapiga kelele kuhusu kusitisha sherehe za Uhuru na fedha zake kuelekezwa kwenye ujenzi wa barabara ya Morocco -Mwenge.

Kutokana na hilo amesema wote waliokuwa wanapiga kelele kuhusu fedha za sherehe hizo sasa wanawahi kufika ofisini kuliko ilivyokuwa hapo awali.

Aitha ameelezea masikitiko yake kwa watu kujielekeza mno katika masuala ya udaku ambayo hayana tija kwa taifa na hayaongeze chochote, hayatusaidii chochote na ndio yanayochukua muda mwingi, kufuatia hilo amesema "tuzungumze uchumi, tujielekeze katika mambo ya maendeleo ambayo hayana chama na nimefurahi kumuona mstahiki meya ambaye ni wa CHADEMA"

Pia aliongeza kwa kusema "Kampeni zilishakwisha, ulie ugalegale Rais ni Magufuli. Ndio maana hii interchange inajengwa kwenye jimbo la Chadema na nawaomba watanzania wa vyama vyote tujielekeze kwenye suala la maendeleo, aliongeza kwa kusema “mnaangaika kwa kuposti kwenye vipost vyenu, mpaka watu wengine wanaingilia uhuru wangu, mimi huwa sipangiwi mambo”.

Alisisitiza kuwa yeye ni Rais anayejiamini na huwa awezi kupangiwa maana hata siku ya kuchukua fomu alienda mwenyewe, hivyo ataamua mwenyewe nani akae wapi, kwa hivyo alisema “Makonda wewe chapa kazi, nasema chapa kazi, nafahamu wamenielewa kama ni kuandikwa kwenye mitandao haina tija, hata mimi naandikwa sana kwenye mitandao kwahiyo nijiuzulu Uraisi?


Hata hivyo Rais aliongeza kuwa angefurahi endapo kwenye mitandao watu wangekuwa wanatoa ushauri kuwa nini kifanyike na siyo kujadili personality badala ya ideas na alisem tuchape kazi kwa manufaa ya watanzania wote.

Post a Comment

 
Top