0
Mkurugenzi wa Clouds Media Ruge Mutahaba ambaye ka nafasi yake anasimamia vipindi, mapema leo asubuhi amezungumza sakata la Kituo hicho kuvamiwa na askali polisi wakiwemo wengine waliovalia magwanda ya jeshi la wananchi nchini uvamizi uliofanyika usiku majira ya saa 5 kasoro ijumaa iliyopita.


DAR ES SALAAM.
Akizungumza kupitia kipindi cha 360 amesema kitendo hicho alichofanya mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda si cha kiungwana ikizingatiwa kuwa kiongozi huyo mkuu wa nchi ni rafiki yao wa karibu, hivyo kwenda katika studio hizo na askali wakiwa na siraha kuliwatia hofu wafanyakazi wa chombo hicho.

“Nilimpigia simu Makonda kumhoji kwa nini aje ofisini na maaskari wenye siraha? Yeye akauliza kwa nini nimezuia kipindi kuruka?, kisha Makonda alikata simu, lakini nilipaniki nikiwaza kuhusu hizo siraha walizokuja nazo ofisini, makonda alisema ‘Bahati yenu’ baad ya kujua kuwa vijana wa SHILAWADU waliokataa kurusha kipindi siyo wao isipokuwa ni mimi” alisema Ruge.

Sakata hilo la mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda kwenda katika kituo hicho kwa kuvamia na askari kimetokana na moja skendo ya kutengeneza ambayo imetokana na mama mmoja ambaye alipiga simu katika kituo hicho na kudai kuzaa ma Bishop Gwajima ambapo baada ya kufuatilia (balance story) inasemekana haikuwa kweli, hivyo kutokana na kitendo cha Bishop Gwajima kumuweka wazi mkuu wa mkoa kuwa hatumii jina lake halisi ahli hiyo imepelekea mkuu huyo wa mkoa kutaka clip hiyo iliyorekodiwa kurushwa ili watu wajue kitendo anachofanya mchungaji huyo wa kondoo.

Aitha Ruge aliendelea kusema kuwa alimpigia simu Kusaga ambaye ni Mkurugenzi wa Clouds Media na kumwambia mkuu wa mkoa ametukosea heshima kwani kulikuwa na aja ganiaje na silaha na ni rafiki yetu?, pamoja na kwamba hakuna aliyepigwa lakini kulijengwa hofu kubwakwa wafanyakazi wa Clouds Media si Jambo dogo.

Ruge alisema “kama watanzania hatutaki kuona kuiona bunduki mitaani, hili limetokea kutufungua macho kujua ma-RC na ma-DC wanavyofanya kazi yao, sisi tuhukumiwe kama taasisi, wafanyakazi wetu wasitiwe hofu, mimi sikuwekwa ndani, nilienda polisi kuripoti suala hili, mtu kuwa na nafasi ya uongozi flani si sababu ya kuwapanda watu, All we want is Respect!”

Kituo hicho cha habari CloudsMedia kinalaani kilichotokea na inaomba vyombo vya Habari vitoe ushirikiano katika kukemea jambo hili.


Post a Comment

 
Top