Mambo mengi yamejitokeza
hivi sasa kuhusu mtu mwenye umri wa miaka 52 ambae aliwaua watu wanne Jumatano
na kuwajeruhi watu zaidi ya 12 wengine katika Daraja la Westminster na ndani ya
Jengo la Bunge la Uingereza.
![]() |
PROFILE
PHOTO: Khalid Masood akiwa anapewa huduma ya
kwanza marabaada ya tukio la mashambulizi.
|
ILIPOISHIA:.... Muuaji huyu alilaumu ubaguzi kwa kupigana kwake, akiiambia mahakama alimkata mmiliki wa mgahawa huo usoni kwa sababu watu wa eneo alilokuwa anaishi katika kijiji cha East Sussex “walimuonyesha chuki” wakati huo alipokuwa anaishi huko.
UPDATE: Endelea hapa,
Jaji aliyemhukumu alitoa angalizo: “Wakati huna
fursa ya kutoa kisingizio chochote kwa tabia yako, inaweza kutoa maelezo kwa
kiwango fulani .”
Lakini tabia yake ya uvunjifu wa amani katika takriban
kesi zote zinazohusu maeneo yote ya umma dhidi yake kwa miaka mingi ziliendana
na tabia yake ya ulevi kabla ya tukio la mwaka 2000 katika ugomvi wa kwenye baa
ambapo alikuwa amekunywa pint nne za bia.
Wakati historia ya utotoni na saikolojia ya Khalid
Masood ina umuhimu kwa wataalamu wa misimamo mikali (na vyombo vya habari vya
Uingereza), ambao wanataka kujua nini kilimpelekea kuuwa, hilo ni jambo dogo
kwa wachunguzi wa polisi ambao wana maswali yanayo husu matukio ya sasa na maswali
muhimu ambayo yanahitaji majibu kati ya hayo, ni lini, kwa nini, na vipi
alikuwa ameingizwa katika misimamo mikali.
Wakati polisi wakipekuwa historia ya Maisha yake ya
siku za nyuma, wanataka kugundua mara moja kama alifanya hilo shambulio kwa
uamuzi binafsi au alikuwa ameelekezwa kulenga Bunge la Uingereza na Je alikuwa
ni sehemu ya mtandao wa watu wenye misimamo mikali ambao wanaendelea na mipango
ya mauaji?
Miaka miwili akiwa Gerezani.
Tarehe za kubadilisha kwake dini kuingia Uislamu
hazijulikani, lakini inadhaniwa kuwa aliingia katika siasa kali wakati
akitumikia kifungo cha miaka miwili kwa kosa la kumkata mtu na panga mwaka 2000
alipokuwa baa,katika nchi kadhaa za
Ulaya, wengi ambao wanaingizwa katika siasa hizo kali ni wale ambao waliwahi kutenda
vitendo vya jinai.
Hakuna mafungamano ya makundi ya wahalifu na kikundi
cha Islamic State au makundi mengine ya wapiganaji lakini yako mafungamano
fulani ya makundi ya kijamii, mazingira na vijana kwa makundi ya wahalifu na
magaidi huwapata wafuasi wao katika makundi hayo, wakitengeneza mahusiano,
wanasema wachambuzi.
Watu ambao walifanya mashambulizi kwenye jiji la Paris
mwaka 2015 na kwenyue jiji la Brussels walikuwa na historia ndefu ya utukutu
utotoni mwao na baadhi yao wanajulikana kuwa waliingizwa katika makundi hayo
wakati wakitumikia kifungo jela, au waliingizwa na watu ambao walikuwa
wameambukizwa siasa kali wakati wakiwa jela.
Tangu siku ya Jumatano polisi wamekuwa wakipekua
nyumba kadhaa ndani ya Uingereza na wamewakamata watu 11 mpaka sasa, wengine
kama ni washukiwa wanaojihusisha na kuandaa vitendo vya ugaidi. Kati ya hao ni
mtu mwenye umri wa miaka 27 kutoka Birmingham na mwanamke, miaka 32, kutoka
Manchester.
“Wote hawa wanahojiwa wakati tukijaribu kuunga vipande
vya taarifa tulizokusanywa katika kile kilichotokea katika shambulio hilo,”
afisa wa ngazi ya juu wa polisi ameiambia VOA. Uchunguzi huo wa polisi,
unaoitwa “Operation Classific” unaongozwa na maafisa kutoka SO15, Kikundi cha
kupambana na ugaidi cha Polisi, Jijini London.
Kaimu Kamshina Msaidizi Mark Rowley Ijumaa amesema:
“Hivi sasa hakuna ushahidi wa tishio lolote zaidi lakini utaelewa kuwa nia yetu
ni kujua iwapo alitenda haya peke yake na kushawishiwa na propaganda za
magaidi; au, watu wengine wamemsaidia, wamempa moyo na kumuelekeza afanye
hivyo.”
Dakika tatu kabla ya kuendesha gari aina ya Hyundai
SUV alioikodi na kuwagonga watembea kwa miguu, alioipeleka upande wao wakati
wanatembea kuvuka daraja la Westminster Bridge, Khalid Masood alikuwa amefanya
mawasiliano na mtu kupitia WhatsApp.
Polisi wanajaribu kumtambu mtu huyo alikuwa ni nani na
walikuwa na mazungumzo ya aina gani.
![]() |
PROFILE
PHOTO: Polisi wa jiji la London wakifanya
uchunguzi kutokana
na tukio la ugaidi la shambulizi lililofanywa
na khalid-Masood.
|
Miaka aliyokuwa Saudi
Arabia
Alikokuwa anaishi katika siku za nyuma kumewafanya
wachunguzi kutaka kujua zaidi. Kwa mujibu wa maafisa wa polisi wa London walio
ongea na VOA, Khalid Masood inasadikiwa aliwahi kuishi kwa miaka kadhaa Saudi
Arabia.
Gazeti la The Sun limeripoti kuwa alihamia nchi hiyo
mwaka 2005 na kwa miaka minne aliwafundisha kiingereza wafanyakazi wa taasisi
ya usafiri wa angani huko Yanbu.
Je, Saudi Arabia ndiko
alikobobea katika msimamo mkali?
Mwaka 2009 alihamia Luton, kaskazini mwa London ambako
tena alikuwa anafundisha Kiingereza, part-time. Kuchagua kwake kwenda Luton
kunaweza kuwa na umuhimu fulani kama ilivyokuwa uamuzi wake wa kuhamia
Birmingham. Miji hiyo miwili imeonyesha wazi kuweko kwa kikundi cha kigaidi cha
Islamic State chenye kuwaingiza raia wa Uingereza kwenye ugaidi.
Washambuliaji waliotumia mabomu July7, 2005 jijini London
walikuwa na mafungamano na mji huo na miji yote hiyo imekuwa ikitembelewa na
wahubiri wenye siasa kali, kwa siku za nyuma akiwemo Abu Hamza, Omar Bakri
Mohammed na Anjem Choudary ambae ni muhubiri maarufu mwenye siasa kali
aliyefungwa mwaka jana kwa makosa ya ugaidi na amehusishwa na njama za kupanga
vitendo vya ugaidi mara 15 tangu mwaka 2000.
Ilikuwa wakati yuko Luton na Birmingham, ndipo vyombo
vya upelelezi vya Uingereza vilipoanza kumfuatilia Khalid Masood, alionekana
pia na majirani zake huko Luton kama “mkazi,” lakini mmoja wa majirani zake
alimuelezea kwa waandishi wa Uingereza alikuwa anaishi kama “kivuli.”
“Sikuwa
namuona mara kwa mara, mara nyingine namuona akitembea usiku, sikuwahi kumuona
mchana kwani ilikuwa tabu kujua anaishi eneo hilo.” Kwa
polisi wa Uingereza wasiwasi wao ni kuwa inawezekana walipitwa na umuhimu wa
kuwatambua “majirani hatari” wengine.
TUISHIE HAPA KWA LEO.
Kwa maoni tuandikie hapo chini kwenye comment au WhatsApp +255773036064
Source
BBC.
Post a Comment