**Chama cha wasindikaji wa
vyakula nchini kimewataka wafanyabiashara wajasiliamali kuongeza ubora wa
bidhaa zao ili kuweza kufikia masoko makubwa hasa ya nje ya nchi hatua itakayo
ongeza nafasi wigo wa biashara na mapato kwa mtu mmoja mmoja na taifa kupata
mapata kutokana na masoko yao.
![]() |
Mwenyekiti
wa shirikisho la wasindikaji wa chakula nchini Suzy Laizer akiongea na wafanyabiashara
wajasiliamali jijini Arusha.
|
![]() |
Aliyesimama
ni Suzy Laizer (Mwenyekiti Taifa), Hulda Kombe (Mwenyekiti Tafopa Arusha),
Restituta Mrosso (Katibu Tafopa Arusha) na Msafiri Mshigheni (Afisa uwekezaji wa jiji -Arusha)
|
![]() |
PICHA
JUU NA CHINI: Baadhi ya wafanyabiashara wa bidhaa za
kusindikwa wakimsikiliza mwenyekiti Suzy Laizer (hayupo pichani) juu ya masoko
na kunyanyua ubora wa bidhaa.
|
![]() |
| Wajasiliamali/Wafanyabiashara wa jijini Arusha wakiwa na bidhaa wanazozalisha |
ARUSHA.
Akiongea na
wafanyabiashara hao jijini Arusha, mwenyekiti wa chama hicho Taifa Suzy Laizer
amewataka wafanyabiashara hao kutumia fulsa zilizopo katika kukuza ubora wa
bidhaa na kuondoka na mawazo ya kusubili msaada kutoka kwa viongozi wanaokwenda
kuwatembelea katika maeneo yao ya uzalishaji.
“wakati umefika kila
mjasiliamali lazima atambue nafasi aliyonayo kutokana na kwamba, kwa sasa
serikali imetoa nafasi kila mkoa kuwa na vikundi vya wakina mama ili kuwawezesha
kukua zaidi kupitia mazao na bidhaa wanazozalisha kufikia ngazi ya juu” alisema Suzy.
Serikali imetenga fungu
la bajeti la asilimia 5 kwa kila halmashauli nchini kuelekezwa kwa kinamama
walio katika vikundi kwa lengo la kuwawezesha kufikia malengo makubwa ya
uzalishaji wa mazao na bidhaa wanazozalisha, hii ni fulsa moja wapo inayoendana
na kaulimbiu ya serikali ya awamu ya tano ya kuelekea kwenye uchumi wa viwanda.
Chama hicho ambacho
kilianzishwa mwaka 1997 kikiwa na kinamama tu ambapo mpaka sasa kinashirikisha
kinababa, kikiwa na lengo la kuleta kwa pamoja sauti ya wasindikaji wa chakula
wa kawaida kuweza kusikika na kukabiliana na vikwazo katika usindikaji wa
vyakula vya viwandani.
Pamoja na
kuanzishwa kwa chama hicho, baadhi ya wafanyabiashara wakubwa na wenye asili ya
asia walikuwa na tabia ya kukataa kupokea bidhaa za ndani zilizozalishwa na
wazalendo huku wao wakiweka bidhaa zilizozalishwa na wao wenyewe au kutoka nje
kwenye masoko makubwa (supermarket)
Wakati huohuo mwenyekiti
Tafopa mkoa wa Arusha Hulda Kombe anayezalisha unga wa mahindi usiokobolewa
(DONA) amewahimiza wafanyabiashara hao kujiunga katika chama hicho ili kuweza
kutambulika na kupata nafasi za fulasa zinazojitokeza ndani ya chama hicho.
“wakati wazalishaji wa
ndani wanazalisha bidhaa bora, hali hiyo ilipelekea kudumiza wazalishaji wa
ndani zikiwemo bidhaa za ndani ya nchi” anasema Hulda.




Post a Comment