Mamlaka ya chakula na dawa nchini TFDA
inaendesha mafunzo ya utoaji wa taarifa za dawa bandia mkoani Arusha kwa
wataalam wa afya nchini ikiwa ni sehemu ya mafunzo yanayofanywa nchi nzima
ikiwa ni sehemu ya kupunguza na kuondoa dawa zisizo halisi katika matumizi ya
dawa zinazotakiwa kutumika kwa binadamu.
![]() |
Kaimu meneja wa Chakula na dawa kanda
ya kaskazini Abdallah Mkanza akiongea na TODAYS NEWS juu ya mafunzo ha utumiaji wa simu
katika kupeleka taarifa za madhara na kuwepo kwa dawa duni bandia.
![]() |
| Mkufunzi wa mafunzo ya matumizi ya program tumishi ya MPRO5 Elia Nyeula akieleza kwa undani juu ya mfumo huo mpya. |
![]() |
Wauguzi na watoa tiba
kutoka mkoa wa Arusha wakifuatilia mafunzo
hayo mapema jana
katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Arusha.
|
![]() |
Madaktari wa wataalam
wa Afya kutoka vituo vya Afya na Hospitali
kadhaa za mkoa wa
Arusha wakiwa makini kufuatilia mafunzo.
|
![]() |
Picha ya pamoja kwa wauguzi, madaktari,
mkufunzi na mgeni rasmi katikati kabla ya kuanza mafunzo hayo jijini Arusha
mwishoni mwa wiki hii.
|
HABARI KWA UNDANI:
ARUSHA.
Mafunzo
hayo ya siku moja yaliyowashirikisha wataalam wa Afya wakiwemo madaktari
na wauguzi kutoka wilaya za mkoa wa Arusha wamepewa ujuzi wa kutambua
dawa duni na bandia huko ziliko pamoja na kuweza kuzipiga picha na kuweza kutuma taarifa kwa wakati kwenda kwaa mamlaka husika kupitia
program tumishi ambayo inapatikana
kupitia mfumo wa simu za kiganjani (smartphone).
“TFDA ikishirikiana na shirika la Afya duniani (WHO) inaendesha mafunzo baada ya kuona kuna umuhimu kutokana na kukua
kwa teknolojia, hivyo matumizi ya kutumia simu za kisasa (smartphone)
yatarahisha mtu kuweza kupiga picha na kuituma kwetu nasi kwa muda na wakati
tutakuwa tumeokoa watanzania wengi ambao wangeweza kutumia dawa hizo duni na
bandia” amesema Abdallah Mkanza
kaimu meneja wa mamlaka ya chakula na dawa kanda ya kaskazini.
Wakati mafunzo hayo yakiwa
ni ya mwisho yakihitimishwa kwa nyanda ya kaskazini baada ya kufanyika nchini
kote, hata hivyo kumekuwepo na malalamiko kutokana na matumizi ya dawa za ARV–TLE
ambazo baadhi ya watumiaji wamekuwa wakiwashwa
na kubabuka baada ya kutumia dawa hizo, tatizo hilo linaonekana ni kubwa
lakini tfda tunaendelea kufanyia
kazi, aliongeza Mkanza.
Mkaguzi wa dawa
kiongozi nyanda ya kaskazini Elia Nyeula anayeendesha mafunzo hayo anasema,
mafunzo hayo yanayowajumuisha wataalam kutoka katika hospitali hapa nchini ni
nzuri na ya haraka katika utoaji wa taarifa hizo muhimu kwa ajili ya
kuhakikisha kuwa dawa duni na bandia zinaondoka.
“kwa nchi za Afrika na dunia kwa ujumla program hii ndiyo
inaanza na itztusaidia sana Tanzania nasi tumechukuliwa kama pirot (viongozi)
ili wengine wajifunze kutoka kwetu. Swala la madawa bandia na yaliyo chini ya
kiwango ni tatizo la kidunia, siyo Tanzania tu lakini kutokana na teknolojia
kuongezeka lakini pia watu kutaka kujiongezea uchumi wao binafsi” anasema
Elia Nyeula.
Aliongeza kuwa
kunapokuwepo kwa dawa bandia kunahafifisha nguvu kazi lakini pia uchumi wa
nchi, ambapo tunapotoa mafunzo haya kwa wataalamu hawa watakuwa ni chachu
kwenye sehemu zao za kazi na kwa taifa kwa ujumla.
Program hiyo tumishi
inapatikana kwa kupakuliwa kupitia simu za kijangani (smartphone) inajulikana
kwa jina mpro5 itaaanza kutumika kwa wataalamu wa Afya ambao watakuwa na namba
maalum ambazo zitawasaidia kuingia na kutoa taarifa.
“Nina imani haya mafunzo yatatusaidia kwani wateja wetu ambao ni
wagonjwa wamekuwa wakilalamika kutokana na kuwepo kwa dawa bandia, hivyo
mafunzo haya yatatusaidia kuweza kutoa elimu vituoni, kutoa taarifa baada ya
kuona madhara ya dawa bandia maana huwezi kutoa taarifa wakati hujaona madhara
yaliyotokana na matumizi ya dawa hizo pia kuweza kuepukana na hili janga” amasema afisa muuguzi msaidi Josebetina
Kamugisha kutoka kituo cha Afya Levolosi Arusha.





Post a Comment