0
PHOTO: Mimbari ya msikiti ikionekana kwa nje.
Toleo moja la muswada huo linapiga marufuku taasisi zote za kidini kutumia vipaza sauti kati ya saa tano na saa moja na toleo lingine linapiga marufuku vipaza sauti vinavyoonekana kuwa na kelele zaidi muda wowote wa siku.

Kulikuwa na hisia kali katika bunge la Israel siku ya Jumatano wakati lilipopitisha sheria kuzuia vipaza sauti miongoni mwa taasisi za kidini, matoleo mawili ya muswada  huo uliojulikana kama ''muswada wa Muezzin'' ambao ungeathiri wito wa ibada miongoni mwa Waislamu 'Adhan' ulisomwa kwa mara ya kwanza na kupitishwa na wachache.


Baadhi ya wabunge wenye asili ya uarabuni walizichana chana baadhi ya nakala za muswada huo wakati wa mjadala uliokuwa na changamoto, hivyo kupelekea muswada huo ambao utalazimika kusomwa kwa mara nyingine na kupitishwa kabla ya kufanywa sheria.
PHOTO: Taswira ya anaye *Adhin kuwakumbusha waumini kwenda kwenda ibada.
Ni marekebisho ya muswada ulioidhinishwa na baraza la mawaziri la Benjamin Netanyahu mnamo mwezi Novemba mwaka uliopita, ambapo Netanyahu alisema kuwa amepokea malalamishi kadhaa kutoka katika jamii zote za Israel kuhusu kelele na matatizo wanayopata kutokana na kelele hizo zinazotoka katika vipaza sauti.

Mmoja ya watu wanaoupigia debe muswada huo Motti Yogev wa chama cha Jewish Home Party alisema siku ya Jumatano kwamba ni muswada unaolenga kuwasaidia raia kupumzika ''Hatuna nia ya kuwaumiza wafuasi wa dini yoyote'', aliongezea.


Wakosoaji wa muswada huo wanasema kuwa unakandamiza wa uhuru wa kuabudu, sauti ya ''Adhan'' haijawahi kusababisha uchafuzi wowote wa mazingira, kwani mojawapo ya tamaduni za dini ya kiislamu na hatujawahi kingilia sherehe yoyote ya kidini inayohusu Judaism.

“Vitendo vyenu ni vya kibaguzi'' ,alionya Ahmed Tibi wa chama cha Joint List alliance chenye Waarabu wengi. ''hatua hii inalenga Uislamu'', aliongezea.

Raia wa Kiarabu nchini Israel wanaojulikana kama waarabu Waisraeli ni kizazi cha Wapalestina 160,000 waliosalia baada ya taifa la Israel kubuniwa 1984, wao ni asilimia 20 ya idadi ya Waisraeli . Asilimia themanini ya Waisraeli Waarabu ni Waislamu na waliosalia wamegawanyika sawa kati ya Wakristo na Druze.



Source bbc.

Post a Comment

 
Top