0
MFUMO WA CHAMA
Mfumo wa Chama, una sura ya serikali na utawala na kuwa na ngazi nyingi ya vikao vya uamuzi. Hali hii inafanya gharama ya kukiendesha Chama kuwa kubwa, vikao haviitishwi na maamuzi ya chama hayawafikii walengwa. Hivyo basi yafuatayo yanazingatiwa,

Na Humphreys Polepole.  -II
Kupunguza wingi wa vikao vya nadharia na badala yake kuwa na vikao vichache vinavyofanyika, vyenye maamuzi yenye tija na kujenga uhai wa chama.

Kupunguza idadi ya wajumbe au wawakilishi ili wawe wachache lakini wenye umakini na uwezo wa kusimamia sera, itikadi, maamuzi ya chama pamoja na kuondoka urasimu na kupunguza gharama za uendeshaji pasina kuathiri ubora wa uwakilishi. Muundo wa Wilaya za Chama uendane na uundo wa sasa wa wilaya za Serikali

Uztio mkubwa umewekwa katika kuimarisha chama katika ngazi ya shina, eneo ambalo ndilo waliko wapiga kura. Kwa kufanya hivyo, chama kitakuwa karibu na watu na watakiona kuwa ni chama chao. Uendeshaji wa shughuli zote za jumuia za chama na mali zake uwe chini ya usimamizi wa Chama cha Mapinduzi na Baraza la Wadhamini la Chama cha Mapinduzi.

VIONGOZI
Viongozi wachache wamekuwa na tabia ya kujilimbikizia nafasi nyingi za Uongozi, utendaji na uwakilishi katika Chama na Serikali. Hali hii hushusha ufanisi na kupunguza tija. Nafasi nyingi kwa mtu mmoja ni kushindwa kuleta ufanisi katika vikao husika.

Hapa imezingatiwa kuwa; ukiacha wale wanaolazimishwa kikatiba kuwa na nafasi zaidi ya moja kwa mujibu wa mamlaka yao, kuanzia sasa nafasi za Uongozi katika chama zitakuwa si zaidi ya moja.

KURA YA MAONI
Mfumo wa kura za maoni hukusudia kuimarisha demokrasia ndani ya chama na kuashiria nafasi ya mgombea anayeonekana kukubalika zaidi, hata hivyo, eneo hili limekuwa na matokeo mabaya ya kukithiri kwa rushwa na kupata viongozi wasio na imani ya kweli ya chama wanaosaka maslahi, wafanyabiashara wenye malengo binafsi na mamluki.

Mapendekezo ya kuimarisha udhibiti wa kura za maoni; -
Katiba ya CCM ya Mwaka 1977 Toleo la 2012 Ibara ya 61A(1-3) inaelekeza kura za maoni za ubunge na uwakilishi zitapigwa kwenye mikutano mikuu ya jimbo na si kwa wanachama wote matawini kama ilivyofanyika mwaka 2015.

Imependekezwa ili kudhibiti taratibu za kura za maoni jimboni, kuepusha migawanyiko, kuziba mianya ya rushwa na kuepusha wapiga kura mamluki, inapendekezwa kufanya mabadiliko ya upigaji kura za maoni za ubunge na uwakilishi pamoja na kufuata utaratibu ufuatao wa kuwajadili wanaogombea;

Wagombea ubunge/uwakilishi watachukua fomu na kurudisha kwa Katibu wa CCM wa Wilaya inayohusika, fomu zote za wagombea ubunge/uwakilishi zitajadiliwa na kutolewa mapendekezo katika ngazi ya wilaya, mkoa na Taifa kabla ya kupigiwa kura za maoni.

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa itateua majina yasiyozidi matatu ambayo yatawasilishwa mbele ya Mkutano mkuu wa Jimbo kwa ajili ya kupigiwa kura za maoni. Mkutano mkuu wa Jimbo utapiga kura za maoni kumpendekeza mwanachama mmoja awe mgombea wa ubunge/uwakilishi katika jimbo hilo.

Mara ya baada ya kura za maoni, mapendekezo ya uteuzi yataanzia kwenye Kamati ya Siasa Jimbo (kwa Zanzibar), Kamati ya Siasa ya Wilaya (Tanzania Bara), Mkoa, Kamati Maalum (Kwa Zanzibar), Kamati Kuu na hatimaye Halmashauri Kuu ya Taifa itafanya uteuzi wa mwisho.

Utaratibu huu hautawapa fursa wagombea kutengeneza makundi na kutoa rushwa kwasababu hakuna anayejua kama atakuwepo kwenye orodha ya wagombea. Wale wana CCM wenye tabia ya kujiandaa na vyama zaidi ya kimoja, kwa utaratibu huu hawataweza kujiandaa mapema kuhamia vyama vingine. Utaratibu huu pia utasaidia kuondoa urasimu na migawanyiko isiyokuwa na sababu.

Aidha, utaratibu huu utahakikisha anapatikana mgombea mwenye msimamo thabiti wa Chama na ni utaratibu halisi kwa chama kuusimamia ipasavyo.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top