Mkutano mkuu wa chama
cha ushirika wa akiba na mikopo cha Tumaini (TUMAINI SACCOS) kimefanyika jijini
Arusha ikiwa ni mkutano wa 27 wa chama hicho tangu kilichoanzishwa mwaka 1990
kikiwa kimekusanya wafanyakazi wa mashirika mawili yasiyo ya kiserikali ya
World Vision, Vision Fund na wafanyakazi wa Tumaini Saccos wakati mpaka sasa kina wanachama wapatao
758 ambao kwa pamoja wanaunda chama hicho cha wa Tumaini Saccos wakiwa ni
waajiliwa kutoka mashirika hayo mawili.
![]() |
Baadhi ya wanachama kutoka kushoto; Joyce Mallya, Alice na Sia wakifuatilia
muhtasari wa mkutano mkuu wa mwaka 2017 jijini Arusha. |
Emmanuel Sanka
akiongea na wanahabari juu ya Tumaini Saccos kilivyofanikiwa katika utendaji
wake kwa miaka takribani 27 kwenye
tasnia ya mikopo kwa
wanachama wake.
|
![]() |
Baadhi ya wanachama
wakiwa makini kufuatilia majadiliano ya
Mkutano mkuu wa mwaka
2017 jini Arusha.
|
![]() |
Wanachama wa chama cha
Tumaini Saccos wakiwa katika mkutano
mkuu wa chama katika mkutano
wa 27 wa chama chao uliofanyika
katika ukumbi wa
Corridor Spring Hoteli jijini Arusha.
|
ARUSHA.
Akiongea
katika ufunguzi wa mkutano huo mkuu wa chama Mrajisi msaidizi wa vyama vya
akiba na mikopo mkoa wa Arusha Emmanuel Sanka
amesema kuwa wakati kukiwa na matatizo kadhaa kwenye baadhi ya vyama vya
akiba na mikopo si kazi raisi kwa saccos kuandaa mkutano mkuu wa mwaka kama
walivyofanya Tumaini Saccos lakini ili linatokana na uongozi madhubuti
unaokuwepo.
“Mimi nawapongeza sana kwa hatua hii kwa sababu vyama vingine
vya Akiba na mikopo wanashindwa kuandaa mkutano mkuu wa mwaka kutokana na
sababu zisizofahamika, lakini niseme jambo moja hapa, wakati kuna walakini
kwenye baadhi ya taarifa za Saccos nyingine, imepelekea mrajisi wa vyama vya
ushirika ameunda tume ili kuchunguza mapungufu yaliyopo hasa ya upotevu wa pesa
za watu, hakuna mtu anayependa kuona fedha ya mtu inapotea lakini tunaangalia
kuona ni namna gani fedha za watu zinalejeshwa” Alisema
Emmanuel.
Wakati chama kumekuwa
na ogezeko utoaji wa mikopo kwa mwaka 2015/16 kwa wastani wa shs 3,291,173,663bilioni
ambapo kiutekelezaji, utoaji huo unaonyesha kuvuka lengo la bajeti kwa asilimia
46%.
Wakati malengo makubwa
ya chama hicho ni kutoa mikopo ya riba nafuu kwa wanachama, Mwenyekiti wa chama
cha Tumaini Saccos Neema Fredrick anasema chama hicho kina mtaji usiopungua 6bilioni
ambazo zinatumika kufanya uwekezaji pamoja na kutoa mikopo kwa wanachama, ikiwa
ni pamoja na kuwa na mfuko wa kijamii unaohudumia wananchama wanapokumbwa na
matatizo ya kijamii kama misiba.
“Urejeshwaji wa mikopo kutokana na tatizo la uchumi kwa baadhi
ya wanachama sisi Tuamaini Saccos bado tupo kwenye hali nzuri kutokana portfolio
ya Tumaini ni 2% kwani taasisi zinazofanya huduma ya mikopo kwa watu zinasema
isizidi 5%, kwa hivyo tupo kwenye hali nzuri ya urejeshaji wa mikopo, lakini
waajili wa mashirika haya mawili World Vision na Vision Fund wanatusaidia
kukata mikopo kutoka kwenye mishahara yao kabla haijapelekwa benki hivyo tuna nafasi
nzuri kwa upande huo” Anasema
Neema.






Post a Comment