0
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Evod Mmanda Herman akifungua mkutano wa kwa niabda ya mkuu wa mkoa wa Mtwara ambaye hakuwepo mapema leo mjini mtwara. 

Wakurugenzi wa wilaya za Mtwara, Tandaimba, Nanyumbu, Masasi na kutoka Lindi wakifuatilia hotuba.

Mganga mkuu wa mkoa wa Mtwara Dr. Lunemo akizungumza mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa utambulisho wa uboreshaji huduma ya Afya.

PICHA JUU NA CHINI: Baadhi ya wataalamu wa Afya na wahudhuliaji wa mkutano huo kutoka wilaya za mkoa wa Mtwara uliofanyika Naf Hotel Apartment mjini Mtwara. 


Wakurugenzi, Madaktari, wakiwemo wawakilishi wa taasisi binafsi zinazojihusisha na utoaji huduma kwa jamii pamoja na viongozi wa serikali wakimsikiliza hotuba za mkutano huo.



MTWARA.
Mkutano wa siku moja  wenye lengo la kuhamasisha uboreshaji wa  afya ya jamii unaofadhiliwa na mfuko wa msaada wa watu wa Marekani unafanyika mkoani Mtwara ambapo umefunguliwa na Mkuu wa mkoa wa Mtwara ambaye aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Mtwara Evod Mmanda Herman ambaye ametanabaisha nafasi ya elimu hiyo kuwa imekuja kwa wakati muafaka.

Akifungua mkutano wa utambulisho wa mradi huo mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa mradu huo wa USAID boresha Afya utajikita zaidi kwenye ufadhili za huduma za VVU na Ukimwi, Kifua Kikuu, uzazi wa mpango, uhamasishaji wa rasilimali, kupambana katika kuweka sawa masuala ya jinsia, ambapo kwenye upande huo wa jinsia mradi unalenga hasa kwa kinamama na watoto pamoja na masuala ya lishe na maboresho kwenye huduma za Afya kwa ujumla.

“mradi huu ni mkubwa nawenye fedha nyingi ambazo kila mkoa unatarajia kupata zaidi ya shs 30bilioni ili kuweza kuendeleza mradi huu ambao unachangamoto mtambuka ndio maana umelenga kwenye hayo maeneo ni kwa sababu yana nafasi muhimu sana katika athali ya Ukimwi, kwa sababu mtu alieambukizwa VVU ni lazima akingwe na magonjwa nyemelezi” amesema DC Herman.
Hata hivyo wakati uboreshaji huo ukihusisha maboresho ya utoaji wa huduma kwa mkoa wa Mtwara bado kuna nyanja kadhaa ambazo zitapewa kipaumbele ni kupitia shirika hilo la USAID pamoja Deloitte ni kufanya kazi pamoja na Halmashauri zote za mkoa wa Mtwara ikiwemo ofisi ya Mganga mkuu wa Mkoa ili kuweza kuwafikia wananchi wengi waliopo sehemu zinazoweza kufikiwa na mradi huo.

Jofrey Tarimo ni Daktari na Meneja wa ufundi wa kanda wa shirika la USAID Boresha Afya anasema  mradi huo utajikita kuweza kupambana na vvu ikiwa ni kuweza kuwasaida wananchi kujikinga na ugonjwa huo, lakini pia mradi utasaidia katika nyanja ya uzazi wa mpango na kuhakikisha wananchi watakao kuwa tayari kupewa huduma na elimu waweze kuipata kwa wakati, sehemu na kupitia mtu sahihi.

Dkt, Geofrey Tarimo amesema “wale wote watakaokuwa tayari kupata huduma hizi tunataka wazifikie bila vikwazo, lakini sula la Maleria tutashugulika nalo ukizingatia Mkoa wa Mtwara ni kati ya mikoa yenye maambukizo ya hali ya juu kwa ugonjwa wa Malaria, ambapo mradi huu wa miaka mitano ulioanza tarehe 01.10.2016 na unatarajia kufanya katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Morogoro, Ruvuma, Iringa na Njombe”





Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top