PROFILE PHOTO:
Dar Es Salaam Regional Commissioner Paul Makonda |
Kitendawili cha elimu pamoja
na vyeti vya mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam imekuwa ni gumzo kwa sasa
ikiwa ni kwenye mitandao ya kijamii na mazungumzo ya watu mbalimbali ambao
wamekuwa wakifuatilia jambo hili na ikiwezekana wengine wakitaka kujua
kulikoni.
DAR ES SALAAM.
Mkuu wa mkoa wa Dar Es
Salaam Paul Makonda amesema kelele zinazoendelea dhidi yake ni sawa ziendelee
kwani ni dalili kwamba vita dhidi ya dawa ya kulevya imefanikiwa.
Makonda amesema hayo
jana alipokuwa mgeni rasmi katika tamasha la Twende zetu Kigamboni jiji Dar Es
Salaam lililofanyika katika wilaya hiyo ambapo alisema mapambano ya dawa za
kulevya ni ya kupona au kufa.
“Mfahamu kuwa tunapambana kati ya mauti na uzima, kelele,
mwangwi vinavyoendelea sasa ni dalili njema kwamba tunaendelea kunyooka” alisema
Makonda.
Dar Es Salaam ya sasa
anaifananisha na chuma kilichopinda na sasa kipo katika hatua ya kunyooka hivyo
lazima zitokee kelelenyingi kama ambavyo zinaendelea sasa, aliongeza Makonda.
“Huwezi kufanya kazi ya kunyoosha chuma bila kusikia mwangi,
kelele na maumivu kwa sababu kazi ya kukomboa vijana dawa za kulevya si rahisi” Alisema Makonda.
Source Habari Leo.
Post a Comment