![]() |
| PROFILE PHOTO: Rais Yoweli Museveni wa Uganda. |
DAR ES SALAAM.
Rais wa Uganda Yoweri Kaguta
Museveni amewasili nchini ikiwa ni ziara ya siku mbili nchini kuanzia leo Jumamosi
lengo kuu likiwa kuimarisha mahusiano ya kiuchumi baina ya Tanzania na Uganda, Museveni
anatarajiwa kuwa na mazungumzo ya faragha na mwenyeji wake Rais Magufuli, pia
atatembelea viwanda vya kampuni ya Said Salim Bakhresa ambaye amewekeza pia
nchini Uganda.
Aidha rais Museveni atatembelea bandari ya Dar es salaam
kujionea utendaji kazi unavyoendelea katika bandari hiyo baada kwa kuwa
asilimia kubwa ya mizigo ya nchi hiyo usafirishiwa kupitia bandari ya Mombasa
tofauti na hapo awali ambapo bandari ya Dar Es Salaam ndio ilikuwa inasafirisha
asilimia kubwa ya mizigo hiyo.
Akizungumza na wanahabari Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano
wa Kimataifa na Kikanda Balozi Dkt Augustine Mahiga amesema mambo mengine ambayo
yataongelewa katika ziara hiyo ya siku mbili ni hatua ambazo zimepigwa katika
ujenzi wa bomba la kusafirishia mafuta gafi kutoka Hoima katika ziwa Albert
Uganda hadi bandari ya Tanga.
Bomba hilo ambalo litakuwa na urefu wa km 1442 na kwa upande
wa Tanzania peke yake litakuwa na urefu wa Km 1147 na baada ya kufika kwenye
bandari ya Tanga ndipo yatasambazwa sehemu mbalimbali duniani na ujenzi wa
bomba hilo unatarajia kutoa ajira kwa watanzania wasiopungua elfu kumi.

Post a Comment