Benki ya First
Natinal Bank (FNB) imezindua tawi jipya mkoani Arusha ikiwa ni hatua moja wapo
ya kukuza uwekezaji kupitia upande wa fedha,ambapo tawi hilo jipya lilipo
katika jengo jipya la PPF Plaza linakuwa ni moja kati ya matawi yake 10 yaliyopo
nchini katika kutoa huduma za kifedha.
![]() |
Naibu waziri wa fedha na mipango Dr.Kijaji
akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi ya benki hiyo.
|
![]() |
Kushoto mkurugenzi mtenadaji Dave Aitken akiangalia Naibu waziri wa fedha na mipango Dr.Kijaji
akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi ya benki hiyo.
|
![]() |
Mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Fabian
Daqarro akisaini kitabu cha wageni ili kuweka
kumbukumbu.
|
![]() |
| Dr. Kijaji na Dave Aitken wakibadilisha mawazo kabla ya tukio la ufunguzi. |
![]() |
Kikundi cha Sanaa cha wa maasai
waliokuwepo kunogesha sherehe za ufunguzi wa tawi hilo jipya kwa kanda ya
kaskazini.
|
![]() |
Wageni waliofika katika sherehe za ufunguzi wa tawi hilo jipya kwa kanda ya
kaskazini, wakipoga picha wamasai (hawapo pichani) kuweka kumbukumbu.
|
![]() |
Vijana wa kikundi sarakasi cha jijini
Arusha hawakusita kuonyesha ujuzi wa wao katika sarakasi.
|
![]() |
Afisa mtendaji wa benki ya FNB Dave Aitken akizungumza wakati
wa uzinduzi wa tawi jipya la benki hiyo mkoani Arusha ambapo alisifu uwekezaji
huo waliofanya kwa upande wa fedha.
|
![]() |
Wafanyakazi wa Benki hiyo kutoka makao
makuu Dar Es Salaam na Arusha wakifuatilia matukio katika ufunguzi huo.
|
![]() |
Naibu waziri wa fedha na mipango Dr. Ashantu Kijaji akiongea na wageni,
wananchi, wafanyakazi waliofika katika ufunguzi wa tawi la Benki ya FNB jijini
Arusha ijumaa iliyopita.
|
![]() |
Baadhi wageni, wananchi waliofika
kuhudhulia ufunguzi huo.
|
![]() |
Meneja wa tawi Edna Kallape akitoa
maelezo kwa naibu waziri wa fedha kuhusu utendaji yakinifu kwa kutumia Simu ya kiganjani kutokea kwenye ATM za tawi hilo.
|
![]() |
Mtaalam wa Computa wa tawi hilo akitoa
maelezo kwa naibu waziri wa fedha Dr. Kijaji kuhusu mawasiliano kutoka benki nyingine kwa kutumia teknolojia iliyopo kwenye tawi hilo.
|
![]() |
Naibu waziri Dr, Kijaji kulia akisisitiza jambo kuhsu utendaji unaotakiwa kwa mtoa huduma za wateja wa benko hiyo.
|
![]() |
Meneja wa tawi Edna Kallape akitoa
maelezo kwa naibu waziri wa fedha kuhusu utendaji yakinifu unaotarajiwa
kufanywa katika tawi hilo.
|
Picha zote na TODAYS PRODUCTION
+255 757 800 307
+255 757 800 307
ARUSHA.
Benki
hiyo imekuwa ikifanya kazi zake katika nchi za kusini mwa jangwa la sahara
tangu mwaka 1874 mpaka sasa inatoa huduma katika nchi za Afrika kusini, Tanzania,
Lesotho, Namibia, Botswana, Zambia, Msumbuji na Swaziland huku ikiwa na mipango
ya kuhudumia watu wengi zaidi barani Afrika.
Akifungua
sherehe fupi na kumkaribisha mgeni rasmi Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo nchini
Dave Aitken amesema wamefungua tawi hilo mkoani Arusha ili kusambaza huduma
ambazo wananchi wanazikosa sehemu nyingine kupitia huduma za kifedha.
“pamoja na kuwepo kwa idadi ya benki
zinazokadilia kufika 60, kutokana na hilo kuna changamoto nyingi kuwafikia
wateja wengi pamoja na kutoa huduma zinazokidhi matakwa ya mteja moja kwa moja,
maana uwekezaji wa fedha unatakiwa kuwafikia wananchi wengi kutokana na maisha
ya watu yanagusa fedha kwa muda mwingi” Alisema David Aitken.
Ameendelea kusema
kuwa katika tawi hilo lilipo barabara ya zamani ya kuelekea Moshi litakuwa na
huduma ya kuweka na kutoa fedha kwa masaa 24 kwa mwaka mzima, pasipo mteja
kupitia kaunta ila ataweza kutumia mashine za kisasa za ATM zenye huduma hiyo, “huu ni
makakati endelevu unaolenga kuhakikisha maeneo mengi nchini yanapata huduma za
kifedha na tawi hili ni kutokana na maslahi ya ukuaji wa haraka wa mkoa wa
Arusha ambao una mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi”aliongeza
David
Naye naibu
waziri wa fedha na mipango Dr. Ashantu Kijaji aliyekuwa mgeni rasmi aliyezindua
tawi hilo azindua tawi hilo alisema, mkoa wa Arusha ukiwa ni mmoja kati ya
mikoa mikubwa kiuchumi na katika ukuaji katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta
ya utalii, uwekezaji wa fedha kupitia benki ni kiashilia kuwa mji unakuwa kwa
kasi.
Dr. Ashantu
Kijaji alisema
“Arusha ina fulsa na hazina kubwaya rasilimali, jambo linalochangia ukuaji wa
haraka wa biashara katika sekta mbalimbali muhimu za kiuchumi, na ni matumaini
yetu kama serikali uwepo wa benki hii ya FNB katika jiji hili utachangia
katikakuleta maendeleo ya biashara za aina yote zikiwepo ndogondogo, za kati na
kubwa kupitia maendeleo na ubunifu wa kibenki”
Tawi la Arusha
linakuja na bidhaa zikiwepo huduma mbalimbali zilizobuniwa mahususi kwa ajili
ya kuwaongezea tija wateja wa kawaida na wafanyabiashara katika kanda ya
kaskazini.



















Post a Comment