![]() |
PROFILE PHOTO: Rais wa Marekani Donard Trump.
|
![]() |
PROFILE
PHOTO: Wachawi waliokusanyika usiku kufanya mambo yao.
|
MAREKANI:
Siku ya Ijumaa majira ya usiku wa manane,
Wamarekani wanaoamini uchawi nchini kote Marekani waliandaa matambiko yenye nia
ya kumuondoa Trump katika nafasi yake urais,
cha ajabu mpaka sasa ukurasa wa Facebook wa matambiko hayo umepata
wafuasi 10,500.
Hatua hiyo imezua ghadhabu kotoka kwa
Wakirsto ambao wamewalaumu wachawi hao kwa kutangaza vita vya kiroho, hata
hivyo wachawi hao wanapanga kurudia tambuko hilo hadi pale Trump atakapoondoka
ofisini/madarakani, ambapo tambiko lingine litafanyika tarehe 26 mwezi
ujao/machi.
Wapinzani wengi wa rais wa Marekani
Donald Trump wanaamini kuwa itawabidi wasubiri kwa miaka minne ili aweze
kuondoka madarakani, hata hivyo wachawi nchini Marekani hawakubaliani na hilo
na kubaini kwamba bw Trump anapaswa kuondoka madarakani kabla ya muhula wake wa
kwanza kumalizika.
Wakati huo huo chama cha Wakiristo nchini
humo kilitangaza tarehe 24 mwezi Februari kama siku ya maombi ya kuukabili
uchawi huo, rais wa Marekani Donald Trump mpaka sasa hajazungumzia lolote
kuhusu mkasa huo.
Source rfi


Post a Comment