Hivi karibu serikali
ilitoa ufafanuzi juu ya ujenzi wa reli ya kisasa ya mwendo kasi itakayojengwa
kutoka Dar Es Salaam mpaka Morogoro kwa hawamu ya kwanza huku fedha za mradi
huo mkubwa zikiwa zinatoka ndani ikiwa ni bajeti ya serikalina siyo mkopo kama
wananchi walivyokuwa wanadhani.
![]() |
| PROFILE PHOTO: Haina uhusianao na habari hii. |
DAR ES SALAAM.
Wakati wa sherehe ya
kumwapisha mkuu mpya wa majeshi ya ulinzi Ikulu jijini Dar Es Salaam Generali Venance
Mabeyo Rais Magufuri alisema, reli hiyo itakayokuwa inatumia umeme itejengwa
kwa shilingi za kitanzania 2 trilioni ambazo ni fedha za Watanzania na wala
siyo fedha za serikali ya Uturuki kama ambavyo vyombo vya habari kadhaa
vililipoti.
Aliongeza kusema kuwa
reli hiyo itakayokuwa na umbali wa kilomita 300 itakuwa na njia kuu pamoja na
njia za mchepuko kwa ajili ya kubeba mizigo, ambapo amelilinganisha reli hiyo
na zile zinazojengwa katika nchi jirani za Kenya na Ethiopia na kusema ni
tofauti kutokana na uwezo wa excel yake inauwezo wa kubeba 25 tani wakati hii
yetu itakuwa na uwezo wa kubeba 38tani “reli hii
tunapanga kuijenga itakuwa ya kisasa zaidi kwani inatumia umeme, sasa kuna watu
wanadhani fedha za ujenzi wa reli hiyo ni za waturuki, hapana ni kwa asilimia
100 ni za serikali”
Vilevile aliweka mkazo
kutokana na umuhimu wa reli hiyo huku akitaka rasilimali na nguvu kazi zote za
serikali ziweze kutumika ili kuwa na mafanikio ikiwa ni pamoja na kutumia rasilimali
watu wafungwa, ambapo kutawexza kupunguza garama za ujenzi, aliongeza kwa
kuagiza kuwa wafungwa washiriki kwenye ujenzi wa reli hiyo kama nguvu kazi kwa “kuponda kokoto,
kusukuma mawe ili wakitoka gerezani wawe safi na wasifanye mabaya tena”
![]() |
| PROFILE PHOTO: Picha ya treni ya Umeme haina uhusianao na habari hii. |
Rais alitaka wafungwa
wafanye kazi kwa misingi ya uzalishaji na siyo kukaa tu wanakula.


Post a Comment