0
Mratibu wa mkutano huo Mueno Udeozor kutoka nchini kenya akiongea katika mkutano wa majumuisho ya pamoja uliofanyika katika hotel ya Naura ijini Arusha.


Wadau wa kilimo kutoka nchi kadhaa wakimsikiliza Mueni Udeozor (hayupo pichani) alipokuwa akitoa mada fupi.


Aliyesimama ni Meaza Melkamu, Mshauri na mtetezi wa sera na utunzaji kwa Afrika, katikati Theresa Rempel Mulaire kutoka Benki ya chakula canada na kulia ni Mueni Udeozor msimamizi wa proglamu za kilimo ukanda wa Afrika mashariki wakimsikiliza.


ARUSHA.
Tabia nchi imekuwa ni sehemu mojawapo inayofanyiwa mijadira mbalimbali kutokana na mabadiriko yanayosababishwa na uharibifu w mazingira ambapo maendeleo ya viwanda kwa nchi zilizoendelea na kwa nchi za dunia ya tatu ukataji wa miti kwa matumizi mbalimbali kubwa likiwa uchomajo wa mkaa hali hiyo inasababisha ukosefu wa mvua kunakopelekea ukosefu wa mvua na upungufu wa chakula.

Mkutano wa tano wa wakulima nchini unaohamasisha ukulima wa kisasa kwa nchi kanda ya Afrika mashariki unaoegemea katika ukulima ndani ya miaka miwili juu ya njia bora za kilimo endelevu unaojulikana kama kilimo hifadhi. Shirika holo lilianza kama benki ya kuhifadho chakula na kukipeleka katika sehemu zenye njaa limeanzisha mradi huu ili kuwasaidia wananchi kujilinda na mabadiriko ya bali ya hewa pamoja na ukulima wa kubifadhi.

Katika mkutano huo ulioshirikisha mataifa zaidi ya 6 za kiafrika ikiwemo nchi ya Canada kupitia shirika la Canadian Foodgrains Bank ambayo ndiyo muandaaji na msimamizi wa mkutano huo, umelenga katika kuwasaidia wakulima wa nchi hizo ili kuweza kujinusuru na uhaba wa chakula unaondelea kuzikumba nchi hizo kutokana na tabia nchi na mazingira


Kongamano hilo kubwa na lenye lengo la kuwapa ujuzi wataalmu mbalimbali wakiwemo maofisa kilimo, wachungaji na watu wengine watakaokuwa karibu ma wananchi utaanza kufanyiwa kazi nchini Tanzania kwa kuanzia na mikoa ya kanda ya ziwa kama Mara, Shinyanga, Geita  na Mwanza ili ikiwa ni sehemu mojawapo ambapo kunaonekana kuna uhaba wa mvua na chakula.

Post a Comment

 
Top