Sakata la watu mashuhuri wanaotakiwa
kuhojiwa na wengine kujipeleka kituo kikuu cha polisi jiji Dar Es Salaam
linaendelea huku tayari viongozi na wafanyabiashara kadhaa wakiwa wamekwenda
kituoni hapo, taarifa zpo nyingi lakini kuna hii ya Mbowe nakuletea hapa.
![]() |
| PHOTO PROFILE: Freeman Mbowe MP. |
DODOMA.
Kufuatia
hatua nyingine mwenyekiti huyo wa taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA
leo katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma amesema hawezi kwenda
polisi kuhojiwa kama alivyoamuru mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam.
Hata hivyo Mbowe amesema atakuwa tayari kutoa
ushirikiano kwa mamlaka zinazohusika ikiwa tu utaratibu sahihi utafuatwa katika
uchunguzi unaotakiwa, vile vile ametishia kuchukua hatua za kisheria dhidi ya
mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda kwa madai ya kumshushia hadhi kama
mbunge na kiongozi mkuu wa upinzani
bungeni akihusishwa na tuhuma hizo za dawa haramu za kulevya.

Post a Comment