0
Moja ya habari kubwa iliyopo wakati huu ikiwa imejiri kuanzia usiku wa kuamkia leo ni kuhusu michezo na hususani ya mataifa ya Afrika iliyokuwa inachezwa mjini Libreville nchini Gabon.

Wachezaji wa Cameroon wakiwa na furaha mara baada ya kukabidhiwa taji. 

Cameroon wamesherehekea toka usiku wote baada ya klabu yao kunyakua Kombe la Afrika la Mataifa AFCON usiku wa Jumapilimjini, baada ya kuilaza Misri mabao mawili kwa moja (2-1)


Ushindi huo unamaliza ukame wa miaka 15 ya Simba wa Cameroon na kusherehekea ushindi wao wa tano ulipatikana kutokana na mkwaju ambao haukutajariwa wa Vinncent Aboubacar uliopigwa dakika mbili kabla ya mchezo kumalizika.


Misri ilifungua mlango wa bao lao la kwanza katika nusu ya kwanza kutokana na goli lililofungwa na mchezaji wa Arsenal, Mohamed Elneny, ambaye aliwapatia Wamisri matumaini ya ushindi baada ya kutoshiriki katika finali hizo tangu 2010.
Wachezaji wa Misri washerehekea bao la kwanza
 Wachezaji wa Misri wakishangilia bao lao walilopata wakati wa kipindi cha kwanza.

Baadaye wachezaji wawili waloingia katika nusu ya kipindi cha pili kwa upande wa Cameroon
Nicolas Nkoulou na Aboubakar walibadilisha mchezo ambapo walifanikiwa kuipatia timu yao ushindi waliosubiri kwa muda mrefu.

Ushindi huo pia ulikuwa kwa kocha wao Hugo Broos, kutoka Ubelgiji aliyekabiliwa na mivutano mikali kutoka kwa vyombo vya habari tangu kuteuliwa kwake mwezi Februari mwaka jana na kuahidi kubadilisha kabisa timu hiyo.

"Mimi hufanya kazi ili kupata matokeo mazuri, na ninafuraha kupindukia kwani tumepata ushindi wa CAN hii leo. Jambo pekee nililowaambia wachezaji na kuwaomba na kwa sababu tulifanya kazi nyingi kwa bidi kwa miezi michachache iliyopita ni kua na subira na kuheshimiana, na nina matumaini vyombo vya habari vitafahamu sasa. Sina tatizo ikiwa mwandishi wa habari ana mkoso na mchezaji wangu au uwamuzi ninaoufanya, au chochote kile,lLakini ni lazima iwe kwa heshima." Manasema kocha wa Cameroon Hugo Broos
Keeper wa Cameroon akiokoa bao
Golikipa wa Cameroon akiokoa moja ya hatari iliyokuwa langoni kwake.
Misri iliyokua na matumaini makubwa kuweza kulinyakua kombe hilo baada ya miaka 10 ya kutoshiriki katika finali hizo ililazimika kuwatumia wachezaji wake wawili wakongwe na wenye ujuzi kwa mafundisho hayo kama Ahmed Fathi na kipa Essam El Hadary waliocheza kwa pamoja kwa mara saba katika finali ya Kombe hilo la Afrika.


"Kwanza kabisa nina wapongeza wachezaji wa Cameroon kwa kunyakua kombe hili, wamecheza vizuri na wanastahili ushindi, bila shaka ninasikitika na kukasirika lakini kusikitika kwangu ni kwa watu wa Misri, kwa hakika nilitaka wawe na furaha hii leo kwa kushinda kombe hili." anasema kocha awa Misri Hector Cuper.

Post a Comment

 
Top