![]() |
Utendaji kazi wa mfumo wa mwili wako kutokana
na vile unavyoulisha na kufanyisha mazoezi.
|
Kushambuliwa kwa kuta za pembeni mwa moyo na ambazo zinaweza
kuzuia damu kupita kwenye mishipa na selli tishu kupata chembe chembe nyeupe (white
blood cell) Atherosclerosis pia ni sababu inayooneka kuwa ya kawaida ya ugonjwa
wa moyo na mishipa. Yote hayo husababishwa na matatizo correctable, kama vile
chakula kibaya, kutokufanya mazoezi, uvutaji wa sigara hata uzito usio wa
kawaida.
![]() |
Moyo ndiyo
kiungo chenye nafasi ya kipekee katika kufanya kazi ya kusukuma damu na kazi
nyingine mwilini.
|
AFYA YA JAMII.
Kulingana na ripoti ya shirika
la Afya Duniani (WHO), inaonyesha robo ya watu wazima waliopo nusu ya nchi za
Afrika ambazo zimefanyiwa utafiti wana angalau sababu tatu zinazoonyesha hatari
zinazoongeza uwezekano wa kuwa na moja au zaidi ya magonjwa ya moyo wakati wa
maisha yao.
Shinikizo la damu ni ugonjwa ambao umeota mizizi
barani Afrika na asilimia zaidi ya 10 ya wananchi wa afrika wanakabiliwa na
ugonjwa wa moyo. Wakati ambapo matumizi ya tumbaku au sigara na pombe yapo
katika kiwango cha chini barani Afrika kuliko sehemu zingine duniani, shinikizo
la damu lipo katika kiwango cha juu zaidi duniani, na kuathiri karibu nusu ya
ya watu wazima.
Kuna njia kadhaa ambazo wataalam wanasema ukitumia
unaweza kuepukana na madhara ya kupatwa na ugonjwa huu endapo utafanya; Mazoezi
ya aina tofauti, kula matunda angalau matano na mboga za kijani kwa siku,
kutotumia tumbaku au sigara na pombe, hizo ni moja ya njia za kupambana na
ugonjwa wa moyo, kansa au kisukari.
Ripoti hiyo inaonyesha kuwa wanawake wa Afrika wenye
umri wa zaidi ya miaka 45 wako katika hatari zaidi ya kuambukizwa magonjwa hayo,
vilevile kiwango hicho kinatisha kwa sababu ugonjwa huo unaathiri pole pole na
mara nyingi unagunduliwa baada ya miaka kadhaa.
Hata hivyo matatizo yote haya ya afya yanaweza kuzuiwa
kwa kula vizuri na kufanya mazoezi, kama tahadhari hizi hazizingatiwi, hali hii
inaweza kupelekea serikali kutumia mabilioni ya pesa katika kugharimia matibabu
ya magonjwa hayo.
Post a Comment