Kufuatia sekeseke la kauli tata za Rais wa Marekani
zisizopendwa na baadhi ya raia wa marekani na wengine kutoka mataifa kadhaa ya
nje ya marekani, hasa baada ya kusaini sheria ya kuzuia waislamu kuingia nchini
humo, kauli hizo zimepelekea hali ya sintofahamu kutokana na upepo kubadirika
kila uchao nchini humo.
![]() |
| Profile: Waandamanaji nchini Marekani wakiwa na mabango yanayomkataa Trump. |
Rais wa
Marekani Donald Trump amemfuta kazi kaimu mwanasheria mkuu Sally Yates masaama
chache tu baada ya kuwaagiza mawakili wa idara ya haki nchini humo kutotetea
uamuzi wa kuwawekea vikwazo raia wanaotoka katika baadhi ya mataifa ya
kiislamu.
Taarifa ya Ikulu ya Whitehouse
imemshtumu mwanasheria huyo kwa usaliti, Sally Yates ambaye aliteuliwa na Obama
alisema kuwa hafikirii kuwa marufuku hiyo iliyowekwa ya muda kwa raia wa
mataifa saba ya Kiislamu ni halali.
![]() |
| Mwanasheria mkuu aliyeachishwa kazi kutokana kutokukubaliana na matamko na sheria anazotoa Trump pia amekuwa akiwaunga mkono waandamanaji. |
Baada
ya kuondolewa katika wadhifa wake nafasi yake imechukuliwa na kiongozi wa mashtaka
kutoka mahakama ya kijimbo ya huko Virginia Dana Boente.
Agizo
hilo la Rais Trump lililotiwa saini Ijumaa iliyopita limesababisha maandamano nchini
Marekani pamoja na nchi za ughaibuni, ambapo hapo awali kundi moja la
wanadiplomasia liliandika barua likikosoa agizo hilo wakisema litazidi
kuhatarisha usalama wa taifa hilo.
Source BBC


Post a Comment