![]() |
Rehema Chalamila enzi zake wakati akiwa kwenye chati ya muziki
wa kizazi kipya ‘aka’ Bongo fleva.
|
DAR ES SALAAM
Wakati
idadi ya wasanii wanaotumia dawa za kulevya nchini ikiendelea kuongezeka huku
vijana wengi na hata ukanda wa Afrika mashariki wakiona ndiyo suluhu ya
kumaliza matatizo yao, Serikali imeanzisha msako dhidi ya wauzaji na waingizaji
wa dawa za kulevya nchini humo.
Hatua
hii ya Serikali imekuja baada ya hivi karibuni kuonekana wimbi la wasanii
wanaotumia dawa za kulevya likiendelea kuongezeka na kutishia mustakabali wa
vijana ambao wamo kwenye tasnia hiyo.
![]() |
Ray C akiwa jukwaani kutumbuiza mashabiki enzi za kiumo hakina mfupa. |
Hivi
karibuni mmoja wa wasanii waliowahi kuvuma sana kwenye muziki Chid Benzi ambaye
hali yake imeendelea kuzorota kutokana na kuathirika kwa kiasi kubwa na dawa za
kulevya, alimaarufu kwa kipindi cha nyuma “unga” na sasa unafahamika kama
“sembe”.
Msanii
huyu licha ya kuwahi kupelekwa katika kituo maalumu kinachotoa huduma kwa watu
walioathirika na dawa za kulevya, mara baada ya kutoka bado hali yake si nzuri,
alirejea tena katika kutumia unga, hali inayomfanya sasa kukosa usaidizi wa
aina yoyote ili kuweza kumnusuru.
![]() |
Huyu ni mwanamuziki
Chidi Benz kushoto akiwa bado hajapata madahara enzi zake na kulia akiwa katika
hali mbaya kutokana na matumizi ya dawa za kulevya.
|
Mbali na Chid Benz, yuko pia msanii wa kike aliyewahi
kuvuma hapa nchini na Afrika mashariki jina maarufu kama “Ray C” Rehema
Chalamila, yeye aliwahi kupokea msaada kutoka kwa aliyekuwa rais wa awamu ya
nne Jakaya Kikwete ambaye alilipia gharama za matibabu yake, lakini nae baada
ya kutoka huko alirejea kutumia unga.
Mbali na wasanii hawa, wamo pia wasaani wengine wengi
wanaoimba, kuigiza na sanaa nyingine ambao nao wanajihusisha na matumizi ya
dawa za kulevya ambazo bila kujua wanajikuta wanashindwa kuacha na kuathirika
pakubwa.
Baadhi ya wananchi wameonesha kuchukizwa na ongezeko
la vijana maarufu kujitumbukiza kwenye matumizi ya dawa hizo, ambazo wanasema
kamwe haziwezi kumaliza matatizo yao bali zaidi ni kuongeza mzigo kwa jamii na
familia zao.
Baada ya kupata taarifa mbalimbali pia kutoka jeshi la poilisi, habari hii inaendelea kwenye kurasa ya tarehe 13.01.2017 >>>>
Post a Comment