0
Mzee Samweli Sitta enzi za uhai wake.
Kilichojiri kwa ufupi wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa spika wa bunge la tisa la Jamhuri la muungano makao makuu ya nchi mjini Dodoma katika ukumbi wa bunge alasiri ya leo.

Mara baada ya kuwasili ukitokea jijini Dar Es Salaam ulipelekwa moja kwa moja bungeni na askari maalum kisha, mara baada ya spika kutoa salaam kadhaa alitoa nafasi kwa waziri wa katiba na sheria Harrison Mwakembe kutoa salamu ambapo hakuweza kumaliza kusoma mara baada ya kutokwa na machozi ya huzuni.


Jijini Dar Es Salaam katika ukumbi wa Karimjee
NAIBU SPIKA: Tulia Atickson ambaye ni naibu spika alisimama na kutoa hotuba kwa niaba ya spika wa bunge la sasa John Ndugai ambapo aliweza kuelezea hatua zote za maisha alizopitia mpaka kifo chake huko nchini Ujerumani alipokuwa akipewa matibabu.
Marehemu Samwel Sitta ameacha mjane ambaye ni mbunge wa urambo mashariki mama Magreth Sitta ambaye walifunga naye ndoa mwaka 1969, na ameacha watoto watano, pia alichaguliwa kuwa spika wa bunge mwaka 2005 ambapo aliweza kuongoza bunge lililokuwa na speed na viwango kama alivyotamka mwenyewe.


Rais mstaafu Jakaya Kikwete akitoa heshima pembeni ya jeneza.
ZITTO KABWE: Pamoja na salamu za upinzani, huku akimtaja kuwa mwanachama kindani wa timu ya simba, alisifu juhudi za marehemu Samweli Sitta akisema alikuwa spika wa watu amabaye aliboresha bunge kupitia uhuru wa kutoa michango bila kubagua vyama, pia alianzisha mfuko wa majimbo, kutetea mkoa wa Tabora na aliwafundisha wabunge namna ya kujibu maswali wawapo bungeni.


TUNDU LISSU: Alianza kwa kumtaja marehemu kama mwamba wa miamba wa bunge, ambaye hakuna kama yeye, ambapo alilifanya bunge kufahamika ndani na nje ya mipaka ya taifa, ikiwa na kulitaka bunge kuwa lenye ‘meno’ uwezo katika maamuzi, likiwa linaisimamia serikali ipasavyo katika uendeshaji wa serikali na ameliweka bunge kwenye ramani ya Tanzania.

SAMSON RWEKIZA: Ambaye ni katibu wa bunge anasema alijuana na marehemu na akiwa kama mzee mwenye hekima na ndiyo maana akapata kufika katika ngazi za juu serikalini.

FREEMAN MBOWE: Kambi ya Upinzani, tulimuona mzee sitta kama kiongozi ambaye hana ubaguzi wa kiitikadi ambaye alisikiliza makundi yote, vilevile alipigania kile alichokiamini, akitetea upinzani wa pale alipoona hapakuwa sawa aliweza kukosoa na pale alipoona serikali inaonewa alikuaw tayari kuitetea.

WAZIRI MKUU: Kassim Majaliwa kabla ya kuhitimisha kazi za bunge alitoa salamu zake alisema marehemu Samweli Sitta alikuwa kiongozi mlezi, mwadilifu, mwenye kuimarisha demokrasia na msema ukweli. Aliweza kuunganisha watu wote na alikuwa mtumishi wa kila mtu, Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina lake na libalikiwe.

SPIKA WA BUNGE: John Ndugai ambaye ndiye spika aliyechukua mikoba ya uspika mara baada ya marehemu mzee Sitta kustaafu nafasi hiyo alisema; Samweli Sitta alisimamia bunge vizuri, pia aliunda bunge linaloisimamia serikali na kuthibiti, lakini pia katika kulitengeneza bunge la tisa ambapo bila kuwasahau wabunge waliomsaidia kulisaidia bunge katika utendaji kama Ndugai, Mwakyembe, Mhagama, Dr. Slaa na wengine.

Kwa mara ya kwanza aliunda kamati ambazo nyingine zilikuwa na wenyeviti kutoka vyama vya upinzani ili kuonyesha uwajibikaji katika shuguli za bunge.

Kisha mwili wa marehemu ulikuwa tayari kwa ajili ya safari ya mwisho kupelekwa mkoani Tabora kwa ajili ya kuhifadhiwa katika nyumba ya milele.


Dawati la habari kutoka TODAYSNEWS Blog linawapa pole ndugu jamaa na watanzania wote kwa tukio hili. 

Post a Comment

 
Top