0

Nembo ambayo itatumika kulitambulisha shirika litakalokuwa linashugulika na afya ya mama na mtoto, linalojulikana kwa jina la Thamini Uhai.


Mkurugenzi mtendaji wa Thamini Uhai Dr. Mwakatundu, akiongea juu ya upungufu wa madawa na nyumba za watoa huduma mapema leo wakati wa utambulisho wa shirika jipya ya Thamini Uhai katika hotel ya Kilimanjaro Kempiski mapema leo jijini Dar Es Salaam.

Dr, Winani kutoka Muhimbili (MoHCDGEC) alipokuwa anagusia mkutano mkuu wa 2005 uliofanyika jijini Paris juu ya sheria za huduma bora na afya ya mama na mtoto mchanga, waliokaa na wakimsikiliza ni viongozi kutoka sekta baadhi, wa kwanza ni mkurugenzi wa Thamini Uhai Dr. Mwkatundu.

Bendi ya muziki ya Wahapahapa ambayo ilikuwepo kutumbuiza muziki wakati wa uzinduzi rasmi shirika Thamini Uhai mapema katika hoteli ya Kilimanjaro Kempiski jijini Dar Es Salaam. 


Mara baada ya uzinduzi wa shirika na mijadara kadhaa ilipigwa picha ya pamoja kwa viongozi wakuu kutoka serikali na taasisi binafsi. Waliokaa kutoka kushoto ni Ms Rose Mlay kutoka White Ribbon Allience Tanzania, Dr.Mwakatundu, Dr Winani, Anna Mswira na Prof. Andrea Pembe kutoka AGOTA

HABARI KWA UNDANI:
Shirika la Thamini Uhai limezinduliwa rasmi leo jijini Dar Es Salaam, shirika hilo ilinalojishugulisha na uokoaji, uboreshwaji wa mazingira na maisha ya wanawake kupata huduma nzuri na zenye ubora kwa uzazi hasa za dharula katika maeneo ya vijijini na maeneo yaliyosahaulika.

Thamini uhai inaweza kujihusisha na uhifadhi ikiwa ni pamoja na kuonyesha idadi ya mambo yaliyomalizika kijiografia, vituo vya afya na hospitali katika wilaya nane mkoani kigoma na pwani tangu mwaka 2008. Kufikia hatua hiyo ya uboreshwaji wa maisha ya mama na watoto wachanga kwa kushirikiana na serikali.

Wakati wa utambulisho rasmi wa jina Thamini Uhai, mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Dr. Mwakatundu amesema chimbuko lake limetokokana na shirika la kimataifa la World Lung Foundation ambalo limekuwa likifanya kazi kwa karibu sana na serikali katika jitihada za kupunguza vifo vya kimama na watoto wachanga tangu mwaka 2008 mkoani kigomma na Pwani.

Wakati shirika hilo likiwa na ushirikiano na serikali pamoja na wadau wengine ikiwa ni kuboresha uwezo na upatikanaji wa huduma timilifu za dharula na uzazi, (COMPREHENSIVE EMERGENCY OBSTRETIC NEONATAL CARE) katika vituo vya afya 19 kwenye maeneo yaliyosahaulika pia imesaidia upatikanaji wa wataalam wenye ujuzi wa juu kwenye uzalishaji wa huduma za dharula.

Hata hivyo mgeni rasmi ambaye ni mwakilishi kutoka hospitali ya muhimbili Dr Winani alisema, katika muongozo wa serikali ambao unalenga kumfanya mtanzania asiweze kutembea zaidi ya kilomita 5, kuwepo na mtaalam mzoefu atakayehudumia kituo husika ili kusaidia upatikanaji wa huduma za kitaalam.

Naye mkurugenzi wa White Ribbon Allience Tanzania Rose Mlay amesisitiza kuwa mara kadhaa bajeti ya vituo vidogo vya afya ambavyo uanzishwa na mashirika mara kadhaa imekuwa ni fedha ya wafadhili ambayo uishia katika uanzishwaji wa vituo hivyo lakini pesa ya uendeshwaji utoka serikalini, lakini serikali utoa pesa pale panapoonyesha kufanya vizuri.


Mjadara kuhusu hali ya afya kwa mama na mtoto inachagizwa kwa wananchi kutambua nafasi ya kila mtu analindwa na mfumo imara wa afya kwa umma, kabla ya hapo inafahamika wagonjwa walikuwa wakikimbizwa hospitali kwa saa tatu au nne kwa hospitali ya karibu, mpaka sasa dharula huduma ya uzazi inapatikana katika jamii.

Post a Comment

 
Top