3

Taasisi ya Lumumba Alliance Club of Tanzania imetoa tamko juu ya wote ambao wanatumiwa na mabeberu ili kuvuruga urithi mkuu tulioachiwa na waasisi wa Taifa letu ambao ni AMANI, UMOJA na UDUGU WA KITAIFA.

Wakati nia na madhumuni ya taasisi hiyo ya Lumuba Alliance Club of Tanzania ni kufanikisha nia njema, maelewano, Amani , maendeleo kwa jamii na kupambana na umaskini, mkuu wa idara ya fedha ndg Mohamed Hussein alitanabaisha taasisi hiyo kutokukaa kimya huku kukitokea watanzania wachahe wanaotumiwa na mafisadi kutaka kuwatenganisha na watanzania na kuharibu nia njema ya kuleta nabadiriko ya kiuchumi  ikiwepo nidhamu katikautumishi wa Umma yanayofanywa na Mh. Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania dr. john pombe magufuri.

Pamoja na kupinga kauli za uchochezi zinazotolewa ndugu Mohammed  alinukuu mmoja wa wanasiasa amabye alitoa kauli inayoonesha wakati wa mfumo wa chama kimoja ambapo hayati baba wa taifa mwalimu Nyerere toka mwaka 1961 hadi 1962 ambapo kulikuwa na majaribio manne ya kumpindua.

Hata LAC inawaomba watanzania wote kwa umoja kulaani kitendo cha baadhi ya makundi hayo huku akigusia lengo la serikali kuhamia Dodoma ambapo amegusia jinsi lengo la kuamisha makao makuu ya nchi na huduma za kiserikali tangu 1973 TANU ilipoanza mchakato kupitia balaza kuu, ambapo tayari baadhi ya ofisi za kiserikali zipo tayari ikiwa na baadhi ya watumishi kupewa fedha za uhamisho japo baadaye walirudi Dar Es Salaam.


Aitha alihoji kauli mbalimbali zinazotolewa na mheshimiwa Rais Magufuri ikiwa ni pamoja na kuwa mkali kuhusu maliasili na utajiri wan chi yetu je, ni Udikteta? Na kuwataka watanzania kujivunia Utaifa na Tanzania haitajengwa nan chi nyingine yoyote bali itajengwa na watanzania wazalendo watakaojitoa mhanga kwa ajili ya Tanzania.
Next
Newer Post
Previous
This is the last post.

Post a Comment

  1. Ni jambo jema kwa taasisi ya lumumba aliance club kuunga mkono jitihada zinazo fanywa na serekali

    ReplyDelete
  2. Ni jambo jema kwa taasisi ya lumumba aliance club kuunga mkono jitihada zinazo fanywa na serekali

    ReplyDelete
  3. Kweli LAC imeonesha Umoja wa kitaifa kwa maslahi ya wengi.

    ReplyDelete

 
Top