0
DAR ES SALAAM. 
Na. Christina Mwagala.
Mkutano wa 33 wa jumuiya ya tawala za mikoa nchini (ALAT) uliokuwa ufanyike jijini Mbeya na baadaye kuhamishiwa jijini Dar Es Salaam umeanza leo kwa baadhi ya wanchama wa mkutano huo kufanya maandalizi yatokanayo na ajenda muhimu zitakazojadiliwa mapema kesho mara baada ya ufunguzi.

PHOTO: Mstahiki meya wa jiji la Dar Es Salaam 
Isaya Mwita (kushoto) akiongea wakati wa
mkutano mkuu wa ALAT jijini Dar Es Salaam.

Mwenyeji wa mkutano wa 33 wa Jumuiya ya Tawala na Serikali za Mitaa ALAT ambaye ni  Meya wa Jiji la Dar es Salaam Isaya Mwita amesema kupitia mkutano huo wataiomba serikali  ili iweze kurudisha vyanzo vya mapato vilivyokuwa katika halmashauri.

Meya Mwita alizungumza kauli hiyo wakati akitoa salamu za kuwakaribisha wajumbe wa mkutano wa ALAT unaofanyika jijini Dar Es Salaam badala ya Mkoani Meya, alisema vyanzo vya mapato ambavyo vilikuwa vikisimamiwa na halmashauri, majiji viliwezesha kuleta maendeleo katika nyanja mbalimbali hususani huduma za kijamii.

Alifafanua kuwa vyanzo hivyo kuwa ni matangazo ya barabarani sambamba na kodi za majego ambapo kwa kiasi kikubwa zilikuwa zikiiletea halmashauri fedha ambazo zilitumika kuboresha huduma za afya, elimu na barabara.

Aliongeza kuwa kwakuzingatia ustawi wa halmashauri hizo ,mkutano huo utajadili na kumfikishia Rais Dk. John Magufuli ili fedha hizo zirudi kwa ajili ya maendeleo hususani Vijijini, Kata na Majiji.

PHOTO: Baadhi ya wanachama, Wakurugenzi, Meya na Maofisa wa wilaya nchini.
“Hali ya Halmashauri nyingi kifedha sio nzuri, na hii ni baada ya vyanzo hivi vya mapato ambavyo tulikuwa tunategemea kuchukuliwa, katika hali yoyote hakuna halmashauri ambayo itakuwa na fedha” alisema Meya Mwita.

Akitolea mfano halmashauri ya Ilala iliyopo jijini Dar es Salaam kuwa kupitia vyanzo hivyo ilikuwa ikikusanya zaidi ya bilioni 68 ambazo zilikuwa msaada mkubwa katika kutoa huduma za kijamii ndani ya halmashauri hiyo.

Aitha alisema kuwa mbali na changamoto za mapato ambazo halimashauri zinakabiliana nazo,alizungumzia changamoto nyingine ni kuhusu hali za madiwani hususani kwenye fedha kuwa imekuwa ngumu.


Alisema “hali ya madiwani kifedha imekuwa ngumu katika utendaji wao  wa kila siku kwasababu wanalipwa shilingi 350,000, ambazo hazitoshi, kutokana na gharama za usafiri anazotumia kuzungukia maeneo yake”

Post a Comment

 
Top