0
Na. Mary Mwakibete.                                                                                 MBEYA.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Gabriel Makalla amefanya ukagua kwenye eneo ambako ujenzi wa meli tatu unaofanywa katika Bandari ya Kyera ambapo amejionea kukamilika kwa moja ya meli hizo ambayo inategemewa kukabidhiwa mwisho wa mwezi huu.


PHOTO: Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makala katikati akiwa na viongozi kadhaa wa mkoa na wataalam wanaofanya ujenzi wa meli tatu katika Bandari ya Kyera mkoani Mbeya.
Ujenzi wa meli hizo tatu unaofanywa katika bandari ya Kyera mkoani Mbeya unatekeleza malengo ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuri katika maendeleo ya sekta ya uchumi pia kuendeleza uchumi kwa kanda ya nyanda za juu kusini.

Katika ukaguzi huo mkuu huyo wa mkoa amesema ujenzi huo wa meli unakwenda sambamba na uhusiano wa nchi zinazopakana na Tanzania na unakusudiwa kukuza mahusiano mazuri yaliyopo ikiwa ni biashara na maendeleo ya haraka kwa nchi hizo jirani kama Malawi wakati uhusiano ukiwa ni mzuri kuliko wakati wowote.

Aitha ameitaka serikali za mkoa wa Mbeya, Njombe na Ruvuma kuboresha barabara zote zinazoingia kwenye bandari hiyo ili kuweka wepesi wa usafiri kuingia na kutoka katika meli hizo na wakati huo huo amewaomba wafanyabiashara na makampuni  kujiandaa kutumia meli mbili za mizigo na moja itakayobeba abiria kwa ajili ya usafiri na usafirishaji wa bidhaa mbali kwa wananchi wa eneo hilo.


Katika hatua nyingine RC Makalla amewataka wananchi kuacha kufanya shughuli za kijamii zinazosababisha kuongezeka na kuharibika kwa mazingira fukwe, kuchimba mchanga na kukata magogo kwenye eneo la bandari hali inayopelekea kupunguza kina cha maji na kuongeza tope bandarini.




Post a Comment

 
Top