Msanii na mwigizaji Wema Sepetu
anayekabiliwa na kesi ya mihadarati, amedai maisha yake yapo hatarini kutokana
na kutishiwa maisha na watu wasiojulikana mara baada ya kutangaza kujiunga na
chama cha chadema.
Wakati huo huo, Wema amedai kukamatwa na kushikiliwa kwa zaidi ya dakika 20 na maofisa wa uhamiaji katika mpaka wa Namanga wakati akitokea nchini Kenya akitumia gari binafsi lenye usajili wa nchi hiyo alilokuwa amekodisha akiwa jijini Nairobi .
Na Joseph Ngilisho -ARUSHA
Kauli hiyo ameitoa jana jijini Arusha
wakati alipomtembelea mbunge wa Arusha mjini God bless Lema kwa lengo la
kumpa pole ambapo alisema hali hiyo imemfanya ajiongeze zaidi kwa kujiimarishia
jeshi lake la ulinzi yeye na mama yake na kudai kwamba hatishiki na
vitisho hivyo na amejipanga kukabiliana navyo kwa hali yoyote ile na yupo
tayari kwa mapambano.
Aidha aliongeza kuwa tangu ahamie chadema
anajisikia amani kwani mzigo aliokuwa nao ameutua na ndio maana hata afya yake
imenawili, amenenepa. "Tangu nihamie chadema Moyo wangu
una amani nahisi nimeutua mzigo mzito sana, nimenawili ndo maana unaona
nimenenepa" Alisema
Wema
Akizungumzia suala la wasanii wenzake
kubeza uamuzi wake wa kuhamia chama cha chadema, alisema hana muda wa
kujibizana na wapumbavu, huo ni uamuzi wake na aliahidi kufanya mambo
makubwa akiwa chadema kwa kutumia nafasi yake ya usanii. Kwa upande wa suala la
mama yake kukamatwa na polisi akidaiwa kutapeli mamilioni ya fedha kutoka kwa
mfanyabiashara Alex Msama,Wema bila kufafanua alisema huo ni mwendelezo ya
mengi yatakayotokea katika kipindi hiki.
Hata hivyo alidai kuwa suala hilo halina
ukweli wowote kwa sababu yalikuwa ni makubaliano yao na kulihusisha suala hilo
na masuala ya kisiasa, ukizingatia kuwa hivi karibuni pia mama yake alivamiwa
na kundi la watu wasiofahamika na kuanza kuponda mawe mengi juu ya nyumba yake
anayoishi peke yake.
"Kiukwe mama yangu sio
tapeli hiyo nyumba inayodaiwa kuwa amemtapeli mamilioni, Alex Msama sio kweli
kwani walikuwa kwenye makubaliano yao na hakuna kesi ya msingi hayo ni mambo ya
kisias tu na tunayatarajia mengi" Alisema
Wema.
![]() |
PHOTO: Wema Sepetu akiwa na mdau wa Chadema Ndaro
Bwire.
|
Wakati huo huo, Wema amedai kukamatwa na kushikiliwa kwa zaidi ya dakika 20 na maofisa wa uhamiaji katika mpaka wa Namanga wakati akitokea nchini Kenya akitumia gari binafsi lenye usajili wa nchi hiyo alilokuwa amekodisha akiwa jijini Nairobi .
Alisema maofisa hao baada ya kulikamata
gari hilo walimhusisha na yeye bila kufafanua sababu za msingi wakati yeye
alikuwa amekodisha kwa ajili ya safari zake na kumfanya asote mpakani hapo
kwa zaidi ya dakika 20 na hivyo kudai kuwa huo ni mpango wa kuendelea
kumdhibiti.
Hata hivyo alisema anajivunia kuingia
chadema akidai chama hicho kina umoja na ushirikiano mzuri na kina wanasheria
mahiri ambao anaamini watamsaidia. Vilevile alisema anafikiria kuhama
nchi iwapo atamaliza salama kesi yake ya dawa za kulevya inayomkabili kwani
amesitishwa na mambo anayofanyiwa ndani ya nchi yake.
Kwa upande wake mbunge Lema alimkaribisha
kwa kishindo Wem na kumtaka aondoe ubishoo kwani awapo chadema atarajie mengi
kumkuta ikiwemo kulala polisi. "Wema karibu sana chadema ila uwe ngangali
mambo ya ubishoo huku hakuna, uwe tayari kulala polisi muda wowote" Alimwosia Lema.


Post a Comment