0
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amezindua mfumo wa kasi wa kampuni ya mawasiliano wa TTCL unaojulikana kama 4G LTE kwa mara ya kwanza mkoani Arusha ikiwa ni sehemu mojawapo ya kuongeza ufanisi, gharama nafuu na huduma kwa wigo mpana wa kampuni hiyo kongwe nchini, ambapo katika uzinduzi huo ulifanyika mapema leo asubuhi ilikuwa ni zawadi kwa mwaka mpya 2017 kwa wakazi wa mkoa wa Arusha na kwa Taifa kwa ujumla.

PHOTO: Mkurugenzi wa Biashara kanda ya kaskazini Simon Marwa akiongea wakati wa kusoma hotuba kwa mgeni rasmi na wafanyakazi wa kampuni kongwe ya mawasiliano TTCL (hawapo pichani) mapema leo jijini Arusha.

PHOTO: Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akionyesha ishara ya T kama uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE mkoani humo ishara hiyo hutumiwa na kampuni ya simu ya TTCL kuzungumizia kizazi cha teknilojia.


PHOTO: Baadhi wa wafanyakazi na viongozi wa kampuni ya TTCL mkoani Arusha wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Arusha Gambo katikati waliokaa.


ARUSHA.
Uzinduzi wa teknolojia hii 4G LTE ni moja kati ya mipango mkakati ulio katika biashara wa miaka mitatu unaolenga kupeleka huduma mpya sokoni na kuongeza tija katika uwajibikaji na huduma kwa wateja ikiwa ni mpango kabambe wa kuboresha miundo mbinu ya kampuni na kuweza kuimarisha mtandao wa simu na data wa kampuni hiyo ambayo ni mhimili wa mawasiliano hapa nchini.

Mkurugenzi wa biashara wa TTCL kanda ya kaskazini Simon Marwa anasema uzindizi wa 4G LTE umeongeza wigo wa mikoa ambayo itakuwa ikipata huduma hiyo ikiwemo, Tanga, Morogoro, Mwanza, Mbeya, Dodoma, Pwani, Dar Es Salaam na kwa sasa Arusha pamoja na visiw vya Unguja na Pemba. “kampuni ya TTCL imepitia mawimbi mengi kiasi cha kuwakwaza wateja wetu na wananchi kwa ujumla, naomba kutumia fulsa hii kuwahakikishia kuwa tumevuka salama mawimbi ambayo yametuimarisha na sasa tumekuwa thabiti zaidi.” Simon Marwa.

Aidha Marwa ameuomba uongozi wa mgeni rasmi Mrisho Gambo akiwa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, kuendeleza umoja katika vita ya kupambana na vitendo vya hujuma vinavyofanywa na baadhi ya watu wenye nia mbaya dhidi ya mbinu miundombimu ya kampuni hiyo ukiwemo mkongo wa Taifa wa MawasilianO.

Wakati huo huo mkuu wa mkoawa Arusha aliyekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo ameipongeza TTCL kwa kuleta huduma hiyo mkoani Arusha ikiwa kwa sasa imekuja ikiwa ni mali ya Watanzania kwa asilimia, ikiwa ni pamoja na mapato na faida yote inabaki hapa nchini kwa sasa.

TTCL ndiyo imebeba jukumu la kuwaunganisha wananchi kwa mawasiliano ya uhakikana inayobeba jukumu la kufanikisha utendaji wa sekta ya mawasiliano pamoja na jukumu la kufanikisha utendaji wa sekta nyingie zikiwemo shuguli za ulinzi na usalama wa nchi.

“Juhudi za Rais wetu mpendwa Mhe Dkt John Pombe Magufuri ambaye mara zote anataka kuona mashirika ya umma yakiwa hai, yakitoa huduma kwa wananchi pamoja na kujiendesha kwa faida kuweza kuchangia katika pato la taifa na ukuaji wa sekta nyingine, hivyo kufanikisha mpango makakati wa Serikali ya awamu ya tano wa kuifanya nchi kuwa ya uchumi wa kati na uchumi wa viwanda” alisema Gambo.

Katika hatua nyingine RC Gambo amewataka watendaji wa TTCL kuacha kuendelea kufanya kazi kwa utaratibu wa kawaida  na mazoea, bali wabadilike ili kuleta mapinduzi, sura mpya na mtazamo mpya wa kampuni kwa jamii. Amesema “kuweni wabunifu, jifunzeni kwa wenzenu waliofanikiwa na hakikisheni kuwa wateja wenu wanaridhika na huduma zenu huku wakiwa mabalozi wenu kwa wengine”




Post a Comment

 
Top