0
Mkutano wa halmashauli kuu ya chama cha mapinduzi NECulioanza hivi karibuni mjini Dodoma kwa kamati kadhaa kukutana na kujadili ajenda muhimu pamoja na kupitisha maazimio ya kuwafukuza baadhi ya wananchama wa CCM waliokwenda kinyume na kukisaliti chama.

DODOMA
M/kiti wa CCM JP Magufuri katkati akiongea.
Mkutano huo umeendelea jana na leo mjini humo ambapo kwa siku ya jana Rais na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi John Magufuri aliweza kuingia katika ukumbi ambako mkutano huo unafanyika mapema kabla ya wajumbe wa mkutano huo wapatao 376 kuingia ukumbini, hali inayokwenda kinyume na Itifaki ya uongozi.

Kutokana na hali hiyo wajumbe wa mkutano huo ambao wengi walikuwa nje wakiongea na wengine kunywa chai na kubadilishana maongezi  walipewa taarifa kuwa Mwenyekiti  ameshaingia ukumbini ndipo baadhi walionekana kutimua mbio na kuacha chai na wengine wakienda kwa haraka kuingia ndani.

Wakati wa kuanza kwa hotuba yake Magufuri alianza kwa kuwapiga viongozi wa chama hicho wa mikoa ambao ni makatibu, wakati wa kumpitisha mgombea wa kiti cha urais hawakumpa ushirikiano mwenyekiti aliyepita Jakaya Kikwete, bali kuna baaadhi ya wajumbe wa NEC walionyesha hisia zao moja kwa moja kwa kuwa na imani na Edward Lowasa, hivyo haoni tija kwa makatibu hao kuwepo katika vikao vya juu kwa sababu kuna wenyeviti wao wanakuwepo.

Akitolea mfano wa balaza la mawaziri ambalo hufanyika pasipo kuwepo kwa manaibu waziri wala makatibu wakuu, lakini ushiriki wao hauathili vikao hivyo.

Pia aliongeza kwa kusisitiza kuwa “wakati wa mkutano kama huu uliopita walisimama na kumpinga mwenyekiti na makatibu mlikuwepo, mbona hamkusimama kumpigania?, na bado watu wakaendelea kuimba wana Imani na mtu fulani”

Post a Comment

 
Top