0
Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo yanategemewa kuitimishwa kesho duniani kote yanatarajiwa kuwashuhudia kinamama wakikusanyika pande zote za dunia ili kuonyesha namna mwanamke anathamani na nafasi yake kutambuliwa katika nyanja mbalimbali.

“Damu nyingi zinapotea kutokana na uzazi kwa kinamama hospitali,
hivyo ni wajibu wangu kama mwanamke kujitolea damu ili kuokoa
maisha ya mwanamke mwenzangu,” anasema Zainab Pazi anayesaidiwa kutolewa damu ambaye ni mkazi wa Kimandoru jijini Arusha, kulia ni sr. Gladness.

Muuguzi kutoka kitengo cha mahabara katika hospitali ya mount
meru Gladness John akimsaidia Seif Omary kutoa damu kwa
ajili ya benki ya damu jijini Arusha.
PHOTO: Sr. Gladness John akihifadhi damu iliyotoka
kwa mwananchi aliyejitolea.

PHOTO: Dr. Gembe kulia akimuhoji mmoja wa wananchi waliofika kupima
Afya katika kiwanja cha Sheikh Amri abeid Arusha, kushoto ni
Sr, Georgia swai, wote kutoka Hopstali ya Mount Meru.

Wakina mama wakiwa katika foleni kuelekea kwenye kipimo cha Saratani.



PHOTO  By; TODAYS PRODUCTION



ARUSHA.
Ikiwa kesho ndiyo kilele chake maandalizi ya siku hii yamekuwa yakifanyika wiki moja nyuma kabala ya siku yenyewe, jijini Arusha maandalizi yamekuwa yakifanyika kupitia hatua mbalimbali ikiwemo kwa taasisi mbalimbali kutoa huduma na bidhaa  mbalimbali katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Mojawapo ni hospitali ya Meru iliweza kuto huduma mbalimbali kwa jamii ikiwa ni kuwapima kinamama magonjwa ya Saratani ya Matiti na Mlango wa uzazi.

“Toka tumeanza kutoa huduma hii tunaona mwitikio kwa kinamama ukiw ni mdogo kulingana na matarajio yetu yalikuwa kuona kinamama wengi wakijitokeza lakini mpaka sasa mwitikio ni mdogo, hivyo tunwaomba kinamama wengi wajitokeze kupata huduma hii ambayo ni bure na inaendelea hata baada ya maadhimisho haya kuisha pale katika hospitali ya mkoa ya Mount Meru kila siku isipokuwa Jumamosi na Jumapili tu.” Anasema Sr. Georgia Swai.

Semina na Elimu juu ya dalili na magonjwa hayo imekuwa ikitolewa sehemu mbalimbali kama Makanisani na misikitini lakini bado mwamko umekuwa ni mdogo sana, hali hii inasababishwa na baadhi ya kinamama kuwa na kazi nyingi ikiwemo biashara ba wengine kusuburi ugonjwa uanze ndipo aende hospitalini.

Dkt Gembe kutoka hospitali ya Meru jijini ARUSHA anasema tunawasaidia kinamama kuweza kugundua dalili za  mwanzo na tunawapa tiba na tiba hii inapatikana mara baada ya mgonjwa kugundulika na dalili za mwanzo kama  Mabaka meupe ambapo tunaanza na tiba mgandisho.

Wakati huduma hiyo ikipatikana uwanjani hapo hospitali hiyo imewasogezea karibu na kuleta huduma nyingine ya kuchangia damu ambapo wananchi wameonyesha hali ya kujali na kumiminika kwa wingi kutoa damu.

Sr. Gladness John kutoka kitengo cha mahabara ya damu hospitali ya Mount Meru anasema, "hakika tumefanikiwa kwa kiwango kikubwa kutokana na wananchi wengi kumiminika na kutoa damu kutokana na kugusawa kwao na hali ya mama mjamzito kufariki kwa kukosa damu, hali hii inatia moyo sana na si kwa kinamama tu wanaojitokeza bali hata kinababa kama unavyoona nao wamekuja kwa wingi"

Post a Comment

 
Top