0
PICHA: Msaidizi wa mkaguzi mkuu wa Serikali Leonard Choti
Sendo akifungua warsha ya mafunzo kwa wakaguzi wa fedha wa ndani
(Internal Auditor) yanayofanyika jiji Arusha.

PICHA JUU: Mkaguzi mkuu wa ukaguzi wa ndani na Mipango
kutoka shirika la JICA nchin Shiro Otomo akitoa maelezo
namna ya handbook sets zinavyofanya kazi.

PICHA CHINI : Shiro Otomo akitoa maelezo kwa wagakuzi namna ya Handbook sets zinavyofanya kazi.




PICHA: Wakaguzi wa mahesabu kanda ya kasikazini wakiwa katika
ukumbi wa mafunzo wakimsikiliza Shiro Otomo (hayupo pichani)
alipokuwa atioa maelezo ya mafunzo.

PICHA CHINI: Wakaguzi wa mahesabu kanda ya kasikazini wakiwa katika
Picha ya pamoja katika chuo cha ufundi Arusha (ATC)

Picha By: Leonard Mutani.    



ARUSHA.
Taasisi isiyokuwa ya kiserikali JICA iliyojikita katika kusaidia nyanja mbalimbali za maendeleo, kijamii, kiuchumi inaendesha mafunzo kwa wataalam wa usimamizi wa fedha Wakaguzi wa serikali waliopo katika halmashauri nchini ili kuweza kuwa na uwezo kwa kutumia njia za kisasa za kukagua ikiwa ni pamoja na muongozo wa vitabu vya mafunzo (handbook sets) na kujua mianya inayoweza kufanya ubadhilifu wa fedha za umma.

Akifungua mafunzo hayo ya siku nne na yaliyoshirikisha wakaguzi wa kanda ya kasikazini, Msaidizi wa mkaguzi mkuu wa Serikali Leonard Choti Sendo amesema kuwa wakaguzi kupata nafasi hii kukuza na kujenga uwezo wao yatawasaidia na kuwahakikishia ubora wenye viwango kwenye utoaji wa huduma, ambapo kwenye mafunzo kama  haya ndipo wanapopatikana wakaguzi wenye weledi katika kusimamia fedha za halmashauri haliyopo.

“Baada ya mafunzo haya, sasa wanaweza kupanga na kufanya kazi zao, kuweka kumbukumbu zao vizuri na kuangalia mapungufu kwa weledi kuliko ilivyokuwa hapo awali, mpaka sasa tupo wakaguzi mabingwa (Champions) 11, lakini kupitia mafunzo haya tunatarajia tutaongezeka na kuwa wengi ili tuweze kuwa imara katika kusimamia fedha za taasisi zetu” amesema Leonard.

Vilevile Mkaguzi mkuu wa ukaguzi wa ndani na Mipango kutoka shirika la JICA nchin Shro Otomo amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuweza kujielekeza kwa umakini katika matumizi ya dondoo za vitabu vinavyotoa muongozo hadidu (handbook sets) lakini kupitia vikundi vya majadiliano hapo ndipo kila mtu ataweza kuuliza au kutoa uelewa kwa kile anachokifaham.


Shirika hili Japan International Cooperation Agency (JICA) lenye makao makuu yake nchini Japan limekuwa likichangia kukuza ushirikiano na wa kimataifa na kutoa nafasi ya kupaza sauti katika maendeleo kwa nchi nyingine ili ziweze kufikia uchumi mkubwa ikiwa ni katika jamii na kuwa na ahueni au utulivu wa kiuchumi kwa kanda zinazoendelea.

Post a Comment

 
Top