0
Benki ya Stanbic Tanzania imezikutanisha Taasisi na sekta mbalimbali za kirahia zisizo za kibiashara na maendeleo katika jamii mkoani Arusha katika msingi wa uwezeshaji wa jamii kuweza kushiriki madhubuti kwenye sekta zao za maendeleo na kuweza kuonyesha kujishugulisha kwa ustawi wa watu na maendeleo na uchumi wa Taifa.


Msimamizi wa washa ya taasisi na sekta binafsi akifungua washa kwa kusisitiza malengo ya na majukumu ya kila muuzuliaji kuweza kujikita katika yale yanayozungumziwa.

Washiriki wa washa wakisikiliza mada ya awali inayoletwa na mleta mada kutoka taasisi ya Angonet ya jijini Arusha.

Abrie Reutenbach Meneja wa kanda upande biashara za nje akitoa maelezo kuhusu utendaji wa benki ya STANBIC kwa ukanda wa Afrika na jinsi ilivyojikita kuwezesha taasisi na sekta ndogondogo.

Katibu mtendaji wa ANGONET Peter Bayo akielezea kuhusiana na majukumu ya taasisi na asasi binafsi zinavyoweza kukuza uchumi kutokana na kuwa na nafasi katika maendeleo ya nchi.

Peter Bayo kulia akimsikiliza Meneja wa Angonet na Meso Petro Ahhm alipokuwa anachangia wakati wa mada iliyogusia wananchi kuweza kutumia nafasi yao kama wazalishaji mali kuangalia na wakati.


Kutoka kulia ni Abrie Reutenbach, Fredric Max, Steven Mpuya na Lawrence Mwandemani wakisikiliza mchango wa Petro Ahhm.

Steven Mpuya Afisa mkuu wa sekta za kijamii akieleza namna ofisi yake kupitia benki ya STANBIC ilivyojikita kuwezesha taasisi na sekta binafsi ili kufikia malengo ya uchumi.

“Kwenye uchumi wa nchi hatuwezi kujitizama sisi enyewew bali hata wengine wanaotuzunguka ikiwa ni pamoja na maendeleo, uchumi unategemea sana kile kinachozalishwa na kuuzwa” alikuwa akichangia Zainul Chandoo ambaye ni meneja wa hazina wa STANBIC Benki Tanzania 

Washiriki wa washa wakisikiliza mada na kufuatilia maudhui yaliyotolewa na waleta mada kutoka kutoka STANBIC Benki jijini Arusha katika hotel ya Mount Meru.

Mameneja wa matawi ya STANBIC wakiwa na meneja wa kanda ya Afrika katika Abrie Reutenbach.

Picha ya kumbukumbu kwa wanataasisi na sekta binafsi kutoka mkoa wa Arusha wakiwa na viongozi mbalimbali wa Benki ya STANBIC katika picha ya pamoja jiji Arusha katika Hotel ya Mout Meru kwenye warsha ya siku moja.

Picha zote na TODAYS PRODUCTION





HABARI KWA UNDANI:

               ARUSHA.
Katika warsha hiyo mkurugenzi wa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Angonet Peter Bayo amesema kuwa pamoja na kuwepo nafasi kwa sekta binafsi kunyanyua uchumi kwa njia ya jamii kujiwekeza moja kwa moja bado sekta hiyo imekuwa nyuma kutokana na kutotambua nafasi yake kiujumla.

Vilevile aligusia uwezeshaji wa asasi na wananchama kuweka mipango yao kama ndoto na maono yao ili wanapoenda kutekeleza mipango yao wawe sawa, “maana asasi nyingi ni taasisi za kijamii hivyo wanapenda baada ya muda na wao waweze kuona wamesogea mbele”.

Lakini wakati hali ya taasisi na sekta binafsi zikiwa hazina uwezeshaji kutokana na kujikita zenyewe pasipo kuangalia nafasi ya kuwatumia viongozi walio katika utashi kitaifa, bado taasisi hizo zinatakiwa kuongea na mamlaka na watoa maamuzi, ikiwa na maana kuna lasilimali ambazo bado hazijaonekana wakati zina mchango mkubwa katika uchumi wa nchi.

Kwa upande wa uchumi Afisa wa fedha wa benki ya STANBIC Zainul Chandoo amegusia kwenye uchumi wa nchi na kusema kuwa taasisi za kiraia zina mchango kubwa japo Taasisi kubwa mbili za Kilimo na Viwanda ndivyo zilizochangia kukuza uchumi mpaka sasa.


“kwa nafasi  hatuwezi kujitizama sisi wenyewe bali hata wengine wanaotuzunguka ikiwa ni pamoja kuangalia maendeleo na uchumi ambao unategemea sana kile kinachozalishwa na kuuzwa, kule kwenye mapato ya serikali (mapato ya ndani) tunategemea taasisi zinazochangia kama taasisi za sekta binafsi ili kuweza kukuza uchumi” alisema Zainul Chandoo.

Post a Comment

 
Top