Mafunzo ya siku tano yaliyokuwa yakitolewa na
Taasisi ya RESCA ikishirikiana na serikali ya Marekani kitengo cha siasa na
kupunguza ueneaji wa siraha nyepesi wametoa mafunzo yaliyohitimishwa leo kwa
maafisa wa jeshi la polisi nchini kutoka mikoa kadhaa ya Tanzania.
![]() |
Mkufunzi mkuu Justin
Pamba akiongea wakati wa kufungua hafla ya kufunga mafunzo ya siku tano kwa
maofisa wa jeshi la polisi nchini yaliyofanyika jijini Arusha.
|
![]() |
Meneja mipango wa
RECSA Godfrey Bagonza pia aliweza kuongea wakati wa kufunga mafunzo hayo huku
akiishukuru serikali ya Tanzania na Marekani kwa kuwezesha mafunzo hayo hapa
nchini.
|
![]() |
Dennis Hadrick Meneja mipango wa idara ya siasa na mambo ya kijeshi kutoka ofisi Marekani akionyesha ramani ya Tanzania wakati wa kufunga mafunzo.
|
![]() |
| Baadhi wa maofisa wa jeshi la polisi waliokuwa katika mafunzo wakimsikiliza Capt Justin Pamba (mbele kushoto) alipokuwa akimkaribisha mgeni rasmi. |
| Mratibu wa taifa wa SALW Charles Ulaya katikati akimkabidhi mmoja wa wahitimu wa mafunzo hayo sgt. Allen Daniel Mbwambo cheti cha maudhulio ya mafunzo hayo ya wiki moja, pembeni ni viongozi waandamizi. |
![]() |
| Dennis Hardrick kulia, Charles Ulaya, WP C. Gerald Minja wa pili kushoto akiwa na cheti cha maudhulio ya mafunzo mara baada ya kupokea cheti pamoja na Godfrey Bagonza. |
![]() |
Picha ya pamoja kwa
viongozi, wakufunzi na wahitimu wa mafunzi ambao ni maofisa wa jeshi la polisi
mara baada ya kukamilika kwa mafunzo na kukabidhiwa vyeti.
|
ARUSHA.
Katika
mafunzo hayo yaliyokuwa yameegemea katika nyanja za utunzaji wa silaha kupitia
maghala na zile zilizopo mitaani ambazo zimekuwa zikitumika kinyume na
matumizi, yameendeshwa na wataalam wa mafunzo kutoka Kenya, Rwanda na Uganda
ambapo kwa siku nne wamekuwa wakiwafunda kwa undani.
Justin
Pamba ni Mkufunzi mkuu wa mafunzo hayo
na mmoja kati ya waliofanikisha mafunzo hayo amesema “pamoja na kuwapa mafunzo hayo na kuwawezesha
kufanikiwa kwa hatua nzuri na muda wote, vilevile malengo tuliyoweka kwa
wahitmu hawa yamekwenda vizuri na kwa muda tuliopanga”
Dennis Hadrick Meneja mipango wa idara ya
siasa na mambo ya kijeshi kutoka ofisi Marekani ametanabaisha jinsi mafunzo
hayo yalivyofanyika kwa ustadi mkubwa wakati ambapo kuwakusanya maofisa wa
jeshi kutoka mikoa yote nchini inaonyesha ukubwa wa Tanzania ambao inahitajika
mafunzo hayo na wahitimu wakayafanyie kazi matokeo ya mafunzo hayo.
"yalikuwa mafunzo muhimu na yenye weledi
wakati wote wa mafunzo ambapo lazima wahitimu muonyeshe kwa wale ambao
hawakufika katika mafunzo kuwa nyie ni tofauti na wao, mnarudi katika viyuo
vyeni vya kazi hivyo mkawe mabalozi na watendaji mtakaowezesha ujuzi mlioupata
ukawe ni chachu ya utendaji wenye tija" alisema Dennis Hadrick.
Watoaji wa mafunzo hayo wametoa kila kitu kwa wahitimu wa mafunzo hayo ili kuhakikisha kuwa kile walichotoa kinaleta nafasi kwa wahitimu kuwa walimu kwa wenzao hususani kwa upande wa utunzaji wa maghala na silaha kwa ujumla.
Akifunga
mafunzo hayo wakati wa utoaji wa vyeti kwa wahitimu wapatao 37 mgeni rasmi Mratibu wa taifa wa SALW Charles Ulaya amewashukuru wakufunzi kwa moyo wa dhati kufanikisha mafunzo na kwa ustadi mkubwa, "pamoja na kuishukuru serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na serikali ya marekani kwa kuunga mkono ambapo SALW imeweza kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi".







Post a Comment