0
Bodi ya wataalamu wa ununuzi na ugavi nchini (PSPTB) inatarajiwa kufanya ziara ya kitaaluma katika mikoa takribani kumi kwa lengo la kuzungumza na umma wa wanafunzi wa vyuo vikuu mbalimbali nchini wanaosomea  fani ya ugavi na ununuzi kwa umma sambamba na mafunzo yatakayofanyika siku ya tarehe 25 februari  mwezi huu jijini Dar es salaam.

Afisa mwandamizi wa Mahusiano ya Umma na Masoko wa PSPTB nchini Shamim Ally Mdee kulia, akiongea wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar Es Salaam kuhusiana na maandalizi, katikati ni kaimu mkurugenzi Godfrey Mbanyi na kushoto Aman Ngonyani.

Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Bodi ya wataalam wa ugavi na ununuzi nchini Godfrey Mbanyi (kulia) akitoa maelezo kwa kina kuhusu elimu ya maadili kwa wanahabari hawapo pichani.

Kaimu mkurugenzi wa mafunzo Aman Ngonyani akiongelea namna mafunzo yatakavyotolewa kwa mikoa kadhaa ili kuweza kuwafikia wanaotarajiwa kufikiwa kwa muda usiopungua miezi miwili. 





DAR ES SALAAM.
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es salaam kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Bodi ya wataalam wa ugavi na ununuzi (PSPTB), Bw. Godfred Mbanyi amesema ziara hiyo inalenga kuwaelimisha wanafunzi wa fani hiyo juu ya maadili ya ugavi na ununuzi wa umma,

Vilevile katika mafunzo hayo yatakayotolewa kwa viongozi wote pamoja na jumuiya za wanafunzi wa ununuzi na ugavi yatawajengea uwezo wa kuwaandaa kulitumikia Taifa kwa uzalendo pindi watakapomaliza.

Aidha bwana Mbanyi ameongeza kuwa ufanyaji wa mitihani ya kitaaluma chini ya mtaala uliothibitishwa na taasisi za kimataifa pamoja na majukumu ya bodi ya usajili kwa kuwajengea uwezo wa kuwa na mawazo chanya ili kujenga uchumi wa viwanda nchini.

Wakati huo huo bodi hiyo inatarajia kuendesha kongamano la siku moja la vijana  ambao wanasomea fani ya ununuzi na ugavi nchini, Sambamba na kongamano hilo, bodi hiyo inatarajia kutembelea vyuo vikuu mbalimbali nchini vinavyofundisha masomo ya ugavi na kutoa mafunzo. Akivitaja vyuo hivyo ni chuo cha usafirishaji (NIT) cha Dar es salaam, CBE Dodoma na Mwanza, chuo kikuu cha Jordani na Mzumbe vilivyopo mkoani Morogoro.


Vyuo vingine ni pamoja na Uhasibu Mwanza, (TIA)Mbeya na Mtwara, St.John na UDOM vilivyopo Dodoma, IAA na Chuo kikuu cha Arusha, SMMUCO na Mocu vya Moshi, Green Bird kilichopo Mwanga Kilimanjaro, RUCU Iringa na SAUTI kilichopo Mwanza na Mtwara.

Post a Comment

 
Top