![]() |
| Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe akiwa na umri wa miaka 93. |
ZIMBABWE.
Hata hivyo, amesema
hakutaka pia "Madam Clinton
ashinde", akirejelea mgombea wa chama cha Democratic aliyeshindwa
uchaguzi wa Novemba mwaka jana Hillary Clinton, "Lakini vilevile, ukija kwa Donald
Trump ambapo anazungumzia uzalendo... Marekani iwe ya Wamarekani, katika hilo,
nakubaliana naye na Zimbabwe iwe ya Wazimbabwe," Bw
Mugabe amesema, kwenye dondoo ambazo zimechapishwa katika gazeti rasmi la
serikali la Herald.
Ameongeza kwamba Bw Trump anafaa
kupewa muda wa kudhihirisha uwezo wake, "Sijui ila mpeni muda bw Trump huenda hata labda
ataangalia upya vikwazo vilivyowekewa Zimbabwe," amesema.
![]() |
| Grace Mugabe kulia akiteta jambo na Mumewe Robert Mugabe kushoto. |
Hivi karibuni mke wa
Rais huyo bi Grace Mugabe ambaye ana miaka 40 akiwa ni umri nusu kwa Mugabe, aliuambia
mkutano wa chama tawala cha ZANU-PF kuwa hata mumewe akifariki, bado jina lake
litawekwa kwenye karatasi za kupiga kura alisema watu wa Zimbabwe wanampenda
Rais wao sana, hivi kwamba wangempigia kura hata akiwa maiti.
Bw Mugabe pia amesema anafaa kuendelea kuongoza, kwani watu
wengi nchini mwake wanahisi kwamba hakuna mtu anayetosha kuchukua pahala pake,
kiongozi huyo tayari ameteuliwa na chama tawala cha Zanu-PF kuwa mgombea wake
wa urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka ujao ambapo ameiongoza Zimbabwe tangu
uhuru mwaka 1980.


Post a Comment