0
Changamoto za maisha, ugumu wa maisha, njaa, hali mbaya ya hewa, mfumo wa maisha, kukosekana kwa ajira na mengine yanayotokea katika baadhi ya nchi yanapelekea baadhi ya raia wa nchi husika kuona hakuna unafuu wa kuendelea kuishi hapo alipozaliwa na hii inatokea mpaka sasa.

Huyu alifichwa kwenye eneo la mbele la gari /dashboard/ ili avuke
mpaka kwenda kutafuta maisha.
Hii ni picha ambayo maofisa walipiga kuonyesha uharisia wa kile kinachotokea
kwa wahamiaji hao, jamaa alifungiwa kwenye sanduku.
Unaweza kupiga picha kupata taswira ni jinsi gani mtu anaweza kukunjwa
na kuwekwa kwenye kiti ili kujificha kwa lengo flani.


CUETA –UHISPANIA.
Maofisa wa polisi wamewakamata raia wawili wa Morocco ambao walijaribu kuwaingiza wahamiaji katika eneo linalotawaliwa na Uhispania lililoplo kaskazini mwa Afrika la Cueta- wawili hao wakiwa wamejificha ndani ya gari na mwengine katika sanduku.
Wakati maofisa hao walipokuwa wanakagua gari moja siku ya Jumatatu, walimkuta mtu mmoja amefichwa kwenye eneo la mbele la gari (dashboard) na mwengine amefichwa kwenye eneo la kiti cha nyuma cha gari.
Mwanamme na mwanamke wanaodaiwa kuwa raia wa Guinea walipewa huduma ya kwanza kwa kuwa walikuwa na hewa kidogo ya kupumua iliyowafanya kuchoka na kudhoofu. Katika tukio lingine kwa raia kuendelea kutafuta maisha kwa kwenda nchi nyingine kwa njia za hatari kijana mmoja mwenye asili ya kiafrika alipatikana amefichwa kwenye sanduku la mwanamke.

Kisa hicho kilitokea mnamo mwezi disemba 30 na mtu huyo anayeaminika kutoka Gabon alihitaji matibabu ya dharura. Vile vile mwanamke mwenye umri wa miaka 22 kutoka nchini Morocco yeye alijaribu kumuingiza Cueta, lakini maofisa wa uhamiaji walimuagiza kufungua sanduku lake ambalo lilikuwa limefungwa kwenye kitoroli.
Kisa hicho kinajili wakati ambapo kumekuwa na majaribio ya wahamiaji wengi kuvunja ugo wa mita sita unaogawanya Cueta na Morocco, raia wapatao 50 wa Morocco na 5 wa Uhispania walijeruhiwa wakati wahamiaji 1,100 walipojaribu kupita wigo huo na kuingia Cueta kutoka Morocco.





Source BBC






Post a Comment

 
Top